Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 2:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 2:14
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mwenye mazarau anatafuta hekima naye haipati, lakini mwenye akili anapata maarifa kwepesi.


Lakini Yesu akageuka na kumwambia: “Ondoka hapa karibu nami, wewe Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa maana mawazo yako si ya Mungu, lakini ni ya kimutu.”


Wengi kati yao wakasema: “Yuko na pepo! Kweli ni mwenda-wazimu! Sababu gani munamusikiliza?”


Ingawa vitambulisho vyote alivyoonyesha mbele yao, hawakumwamini,


naye ndiye Roho wa ukweli. Dunia haiwezi kumupokea, kwa sababu haimwoni wala haimujui. Lakini munamujua, kwa maana anaishi pamoja nanyi naye anakuwa ndani yenu.


Lakini Musaidizi, ndiye Roho Mutakatifu, yule Baba atakayemutuma kwa jina langu, atawafundisha maneno yote na kuwakumbusha yote niliyowaambia.


“Wakati Musaidizi nitakayewatumia toka kwa Baba atakapokuja, atanishuhudia mimi. Yeye ni Roho wa ukweli, naye anakuja toka kwa Baba.


Basi namna gani mutaweza kuamini, ninyi munaopokea sifa kutoka wamoja kwa wengine, lakini hamutafuti sifa inayotoka kwake anayekuwa Mungu peke yake?


Kwa sababu gani hamuelewi maneno ninayowaambia? Ni kwa sababu hamutaki kusikia maneno yangu.


Na kati ya wanawake wale kulikuwa mwanamuke mumoja aliyeitwa Ludia, wa muji Tuatera. Yeye alikuwa muchuuzi wa nguo nyekundu za bei kali na mwenye kuogopa Mungu. Mwanamuke yule akatusikiliza kwa maana Bwana alimufungua moyo kusudi apate kufuata kabisa maneno Paulo aliyosema.


Walimu wamoja wa kikundi cha Waepikurio na cha Wastoiko, wakaanza kubishana na Paulo. Wamoja wao wakauliza: “Huyu katetea anataka kusema nini?” Wengine wakasema: “Anaonekana kuwa muhubiri wa miungu ya kigeni.” Walisema hivi kwa sababu Paulo alikuwa akihubiri juu ya Yesu na jinsi alivyofufuka.


Nao waliposikia Paulo akisema juu ya ufufuko, wamoja wakamuchekelea na wengine wakasema: “Tutakusikiliza tena ukisema juu ya habari hii siku ingine.”


Lakini kwa kuona ni mabishano tu juu ya maneno, majina na sheria yenu, maneno yale yanawaangalia ninyi wenyewe. Mimi sitakata maneno yale.”


Walikuwa tu wakibishana naye juu ya dini yao wenyewe na juu ya mutu mumoja aliyeitwa Yesu; lakini Paulo alidai kwamba yuko muzima.


Hivi, mahubiri ya kufa kwa Kristo juu ya musalaba yanahesabiwa kuwa upumbafu kwa wale wanaopotea. Lakini kwa sisi tunaookolewa ni uwezo wa Mungu.


Mungu alikusudia kuwaokoa wale wanaomwamini kwa njia ya mahubiri tunayotangaza yanayoonekana kuwa mambo ya upumbafu. Amefanya vile kwa sababu, kwa njia ya hekima yao ya kimutu, watu hawakumutambua Mungu na hekima yake ya kimungu.


Lakini sisi tunamuhubiri Kristo aliyetundikwa juu ya musalaba, na mahubiri hayo yanahesabiwa kama kikwazo kwa Wayuda na upumbafu kwa watu wa mataifa mengine.


Kwa maana mambo wanayomuhesabilia Mungu kuwa ya upumbafu, yanapita hekima ya watu; nayo mambo yale wanayomuhesabilia kuwa ya uzaifu yanapita nguvu za watu.


Wakati unapozikwa ni mwili wa kimutu, lakini unapofufuka unageuka mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa kimutu, basi kuna mwili wa kiroho vilevile.


Si mwili wa kiroho unaotangulia lakini ni mwili wa kimutu, kisha ule wa kiroho unafuata.


Na sisi hatukupokea roho ya dunia hii, lakini tulipokea Roho anayetoka kwa Mungu, kusudi tupate kujua vitu vyote tulivyojaliwa kwa neema ya Mungu.


Kweli wandugu zangu, sikuweza kusema nanyi kama watu wanaotawaliwa na Roho wa Mungu, lakini kama watu wanaotawaliwa na mambo ya kidunia. Mungali kama watoto wachanga katika mambo ya Kikristo.


Hekima ya namna hii haitoki mbinguni; lakini ni ya dunia, nayo ni ya kimwili na ya kishetani.


Lakini munajazwa na Roho Mutakatifu ambaye Kristo alimimia juu yenu, na kwa hiyo ninyi wote munajua ukweli.


Lakini Kristo amemimia Roho juu yenu. Na kufuatana na vile Roho yule anavyokaa ndani yenu, hamuhitaji kufundishwa na mutu, kwa maana Roho wake anawafundisha mambo yote. Roho yule anasema ukweli wala hasemi uongo. Basi kama vile Roho alivyowafundisha, mukae ndani ya Kristo.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


Watu hawa ndio wanaoleta matengano; wanatawaliwa na tabia za kimwili nao hawana Roho wa Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ