Namani, jemadari wa waaskari wa mufalme wa Aramu, alikuwa mutu mukubwa aliyeheshimiwa sana na bwana wake, maana kwa njia yake Yawe aliiletea inchi ya Waaramu ushindi. Alikuwa askari hodari, lakini alikuwa na ugonjwa wa ukoma.
Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”
Mungu ashukuriwe kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo! Basi hivi kwa upande mumoja ninatumikia sheria ya Mungu kwa akili yangu, lakini kwa upande mwingine ninatumikia sheria ya zambi kwa hali yangu ya kimwili.
nanyi wenyewe mutatusaidia kwa njia ya maombi. Kwa hivi Mungu atajibu kwa maombi yaliyotolewa na watu wengi kwa ajili yetu na kututendea wema, na watu wengi watamushukuru kwa ajili yetu.
Lakini Mungu ashukuriwe, maana yeye ndiye anayetupatia ushindi siku zote katika ushirika wetu pamoja na Kristo. Anatutumia sisi kwa kutambulisha Kristo pahali pote kama vile harufu nzuri ya marasi inavyosambaa popote.
Basi kwa kuwa hao watoto ni wanadamu, wenye mwili na damu, Yesu vilevile alitwaa ile hali ya mwanadamu. Alifanya hivi kusudi kwa njia ya kufa kwake amwangamize Shetani aliyekuwa na uwezo wa kuleta lufu.