Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 15:52 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

52 kwa rafla, kama vile mutu anavyofunga jicho na kulifungua, wakati ngunga ya mwisho itakapolia. Kwa maana wakati itakapolia, wafu watafufuka na kupata kuwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi wote tutabadilishwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 15:52
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wanaangamizwa kwa rafla, wateketezwe kabisa kwa vitisho.


Basi, siku ya tatu asubui, kukatokea ngurumo na umeme na wingu zito juu ya mulima. Kukasikilika vilevile sauti kubwa ya baragumu ambayo iliwatetemesha watu wote katika kambi.


Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kusikia sauti ya baragumu juu ya mulima uliokuwa unafuka moshi, wote wakaogopa na kutetemeka. Wote wakasimama mbali,


Walifanya hivyo maana Yawe alikuwa amemwambia Musa: Uwaambie Waisraeli: Ninyi ni watu wenye vichwa vigumu. Nikienda pamoja nanyi kwa muda mufupi tu, nitawaangamiza. Hivyo muvue mapambo yenu kusudi nijue namna ya kuwatendea.


Enyi wakaaji wote katika ulimwengu, nanyi munaojaza dunia! Bendera itakaposimikwa kwenye mulima, muangalie! Baragumu itakapopigwa, musikilize.


Siku hiyo, baragumu kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea katika inchi ya Asuria au waliotawanywa katika inchi ya Misri watarudi na kumwabudu Yawe juu ya mulima mutakatifu kule Yerusalema.


huyo anapoona waadui wanakuja, atapiga baragumu na kuwaonya watu.


Lakini kama yule mulinzi akiona waadui wanakuja naye hapigi baragumu na watu wakikosa kuonywa juu ya hatari inayokuja, waadui wakikuja na kumwua mutu yeyote kati yao, huyo mutu aliyekufa, atakuwa amekufa kwa kosa lake. Lakini mimi nitamulaumu mulinzi kwa kifo cha mutu huyo.


Yawe atawatokea watu wake; atafyatua mishale yake kama umeme. Bwana wetu Yawe atapiga baragumu; atafika pamoja na upepo mukali wa kusini.


Lakini kama ikipigwa baragumu moja tu, basi ni viongozi tu wa makabila ya Israeli watakaokusanyika karibu nawe.


Mujitenge na watu hawa, niwaangamize sasa hivi.


Baragumu kubwa itapigwa, halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, kusudi wawakusanye watu wake aliowachagua, kutoka katika dunia nzima.


Kweli, kweli ninawaambia: kutakuwa wakati, nao umekwisha kutimia, wafu watakaposikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale wanaoisikia, wataishi.


Musishangae kwa ajili ya maneno haya, kwa sababu kutakuwa wakati wafu wote wanaokuwa ndani ya makaburi watakaposikia sauti yake


Lakini kila mutu atafufuka kufuatana na utaratibu wake; Kristo ndiye anayekuwa wa kwanza, na kisha watu wake watafufuka, wakati atakaporudia.


Itakuwa hivi vilevile wakati wafu watakapofufuka. Mwili unazikwa katika udongo katika hali ya kuharibika, lakini unapofufuka, unafufuka na hali ya kutoweza kuharibika


Wandugu zangu, muangalie, jambo ninalotaka kusema ni hili: kile kilichoumbwa kwa nyama na damu hakiwezi kupata urizi katika Ufalme wa Mungu katika hali ile, wala hakuna chenye hali ya kuharibika kinachoweza kuwa na hali ya kutoharibika.


Kwa maana, kufuatana na mafundisho ya Bwana, tunawaambia hivi: sisi tutakaokutiwa wazima wakati Bwana atakaporudia, hatutawatangulia wale waliokufa.


Siku Bwana atakaporudi, itatimia kama vile mwizi anavyokuja. Siku ile mbingu zitatoweka kwa shindo kubwa, na viumbe vyote vinavyoangaza katika mbingu vitayeyuka. Dunia na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake vitateketezwa.


Kisha nikaangalia tena, nami nikasikia tai mumoja akiruka juu sana katika anga akisema hivi kwa sauti kubwa: “Ole! Ole! Ole kwa wakaaji wa dunia, kutakaposikilika mulio wa zile baragumu zingine ambazo wamalaika watatu wanatayarisha kupiga!”


Kisha nikaona wamalaika saba wakisimama mbele ya Mungu, nao wakapewa baragumu saba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ