Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 15:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Basi ikiwa kweli wafu hawatafufuka, Kristo vilevile hakufufuka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 15:13
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na kama Roho wa Mungu aliyemufufua Yesu anakaa ndani yenu, basi huyo aliyemufufua Kristo ataupatia mwili wenu unaokuwa wa kufa uzima kwa njia ya Roho wake anayekaa ndani yenu.


Tunaamini kwamba Yesu alikufa na alifufuliwa, na kwa hiyo tunaamini vilevile kwamba Mungu atawafufua pamoja na Yesu wale waliokufa wakimwamini Yesu.


Mimi ni mwenye uzima. Nilikuwa nimekufa, lakini sasa mimi niko muzima kwa milele na milele. Niko na mamlaka juu ya lufu na kuzimu.


Tumusifu Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kubwa ametupatia uzima mupya kwa njia ya kumufufua Yesu Kristo. Na kwa hiyo tumepata tumaini lenye uzima,


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Basi kwa kuwa hao watoto ni wanadamu, wenye mwili na damu, Yesu vilevile alitwaa ile hali ya mwanadamu. Alifanya hivi kusudi kwa njia ya kufa kwake amwangamize Shetani aliyekuwa na uwezo wa kuleta lufu.


Tangia sasa nimetayarishiwa zawadi ya ushindi, ndiyo ile taji ya haki, ambayo Bwana anayekuwa Mwamuzi wa haki atakayonipa siku ile ya kurudi kwake. Wala hatanipa mimi peke yangu tu, lakini na wale wote wanaopenda kumwona wakati atakaporudi.


Lakini, kwa hakika Kristo amefufuka na hii inahakikisha kwamba wale waliokufa watafufuliwa vilevile.


Na si viumbe hivi tu; hata sisi tuliokwisha kuwa na Roho wa Mungu kama sehemu ya kwanza ya zawadi Mungu atakazotoa, tunaugua vilevile ndani yetu, tukingojea kukubaliwa na Mungu kuwa watoto wake, maana yake kukombolewa kwa kimwili.


(Ilitokea vile kwa maana Wasadukayo wanasema kwamba wafu hawatafufuka na kwamba hakuna wamalaika, wala roho; lakini Wafarisayo wanakubali mambo hayo yote.)


Ikiwa tunahubiri kuwa Kristo amefufuka, namna gani basi wengine kati yenu wanasema kama wafu hawatafufuka?


Na kama Kristo hakufufuka, mahubiri yetu ni ya bure na kuamini kwenu ni kwa bure vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ