Kwa maana tumeokolewa, lakini ni kwa tumaini. Mutu akiona kitu anachokitumainia, hilo si tumaini tena, kwa maana nani anayeweza kuendelea kutumainia kitu anachokiona?
Ikiwa wengine wako na haki ya kupata vitu kama vile toka kwenu, sisi hatuna haki zaidi kuliko wao? Sisi hatudai kutendewa sawa na haki yetu, lakini tunavumilia kusudi tusiiwekee Habari Njema ya Kristo kizuizo chochote.
Kufuatana na ile, sisi tunajivuna kwa ajili yenu katika makanisa ya Mungu kwa sababu ya uvumilivu wenu na imani munayokuwa nayo katika mateso na taabu munazopata.
mateso na taabu yangu. Unajua mambo yote ambayo yalinitokea kule Antiokia, Ikonio na Listra. Mateso haya niliyavumilia, na Bwana akaniokoa katika yote.
Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.
Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.