Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 13:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Upendo unavumilia, ni wenye wema; upendo hauna wivu, upendo haujivuni, na hauna kiburi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 13:4
53 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Rakeli alipoona kwamba hajamuzalia Yakobo watoto, alimwonea Lea dada yake wivu, akamwambia Yakobo: “Unipatie watoto, kama sivyo, nitakufa.”


Wandugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akakuwa anafikiri juu ya jambo hilo.


Wakakataa kutii; hawakukumbuka maajabu uliyofanya kati yao. Wakakuwa wagumu, wakajichagulia kiongozi wa kuwarudisha katika utumwa katika inchi ya Misri. Lakini wewe Mungu uko mwepesi kwa kusamehe, mwenye huruma na rehema, haukasiriki upesi, uko mwema sana. Haukuwatupilia


Njia za mwovu zinafanikiwa siku zote; hukumu zako ziko mbali na mawazo yake, na anazarau waadui zake wote.


Chuki inaleta ugomvi, lakini upendo unafunika makosa yote.


Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.


Kuanzisha ugomvi ni kama kufungua maji ya kisima; achana na ugomvi mbele haujafurika.


Anayesamehe makosa anajenga urafiki, lakini anayekumbusha makosa anatenga warafiki.


Kitu kinachotakiwa kwa mutu ni uaminifu; afazali mutu masikini kuliko mutu mwongo.


Anafungua mukono wake kwa kuwapa wamasikini, ananyoosha mukono kwa kusaidia wakosefu.


Anafungua kinywa kwa kusema kwa hekima; anawashauri wengine kwa wema.


Mutawala akikukasirikia, usiache kazi; makosa makubwa yanaweza kufutwa ukiwa munyenyekevu.


Alisema vile kwa maana alijua kwamba walimutoa Yesu kwake kwa sababu walimwonea wivu tu.


“Wale babu wakamwonea Yosefu wivu hata wakamwuzisha kuwa mutumwa katika inchi ya Misri. Lakini Mungu akamulinda,


Wamejaa kila namna ya uovu, ubaya, tamaa na upotovu. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na ukorofi. Wao ni wenye kuchongeana,


Tukuwe na mwenendo muzuri unaostahili wakati wa muchana, tukijilinda na ulafi na ulevi, uasherati na uzinzi, magombano na wivu.


kwa sababu mungali munatawaliwa na mambo ya kidunia. Kwa maana ikiwa kungali wivu na ugomvi katikati yenu, haionyeshi kwamba munatawaliwa na mambo ya kidunia, nanyi munaishi kufuatana na hali ya kimutu?


Watu wamoja kati yenu wanajivuna wakifikiri kwamba sitakuja kuwaona.


Wandugu zangu, nimesema maneno haya nikitwaa mufano wa Apolo na wangu mimi mwenyewe kusudi yakuwe fundisho kwenu. Nilitaka kwamba kufuatana na mufano huu mujifunze maana ya masemi haya: “Musipite pembeni ya maandiko.” Hata mutu mumoja kati yenu asijivunie mutu fulani na kuzarau mwingine.


Nanyi munajaa na kiburi. Ninyi mungepaswa kuhuzunika na mutu yule aliyefanya kile kitendo, naye angepaswa kutengwa toka katikati yenu.


Sasa tuangalie mambo yanayoelekea nyama zinazotolewa kwa kutambikia sanamu za miungu: tunajua kwamba “sisi wote tuko na elimu,” kama vile munavyozoea kusema. Elimu inamufanya mutu kuwa na kiburi, lakini upendo unawajenga watu katika imani.


Kwa maana ninaogopa kwamba wakati ninapokuja kwenu, sitawakuta sawa vile ninavyotaka, nanyi hamutanikuta sawa vile munavyotaka. Ninaogopa kuwakuta katika fitina, wivu, kasirani, ugomvi, masingiziano, matetano, majivuno na fujo.


Tunaonyesha kwamba sisi ni watumishi wa Mungu kwa njia ya usafi wa moyo wetu, ya ufahamu, ya uvumilivu, ya wema wetu, ya Roho Mutakatifu, ya upendo wetu wa kweli,


Tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.


Mukuwe wanyenyekevu kabisa, wapole na wavumilivu. Muvumiliane ninyi kwa ninyi kwa upendo.


Lakini mutendeane wema ninyi kwa ninyi; musameheane kama Mungu alivyowasamehe ninyi kwa njia ya Kristo.


Ni kweli kwamba wengi kati yao wanahubiri habari za Kristo kwa wivu na ugomvi, lakini wengine wanahubiri katika nia nzuri.


Mungu atawatia nguvu kwa uwezo wake wenye utukufu, kusudi mupate kuvumilia kila kitu pasipo kuchoka. Basi kwa furaha,


Musikubali kuhukumiwa na mutu yeyote anayejionyesha kwa inje kuwa yeye ni munyenyekevu na mwenye kuabudu malaika. Mutu wa namna hii anatia sana maana juu ya maono anayopata, naye anajitapa bure juu ya mafikiri yake ya kimutu.


Ninyi ni watu wa Mungu, yeye amewapenda na kuwachagua kwa ajili yake mwenyewe. Kwa hiyo, mukuwe na moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.


Tunawasihi wandugu, muwaonye wale wanaokuwa wavivu, muwatie moyo wale wanaoregea, muwasaidie wale wanaokuwa zaifu, na mukuwe wavumilivu kwa watu wote.


yeye anajaa majivuno wala hajui kitu. Yeye yuko na ulema wa kubishana na kugombezana juu ya maana ya maneno. Na hayo yanaleta wivu, makelele, matukano, masingiziano


Anapaswa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye; kwa maana labda Mungu anaweza kuwajalia hata wapate kugeuka toka zambi na kutambua ukweli.


Lakini wewe umefuata kabisa mufano wangu katika mafundisho yangu na mwenendo wangu, makusudi yangu, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, ungojevu wangu,


utangaze Neno la Mungu kwa nguvu kwa wakati unaofaa na kwa wakati usiofaa. Ukaripe, usahihishe na kuonya ukifundisha kwa uvumilivu.


Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.


Musizani kwamba ni kwa bure Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anasikia wivu sana kwa ajili ya yule Roho aliyemuweka akae ndani yetu.”


Basi, mutupilie mbali matendo yote maovu na ya udanganyifu pamoja na wivu na masingizio ya kila namna.


Kwa kumaliza, ninyi wote mukuwe na mawazo na nia moja, mupendane kama wandugu waamini, mukuwe wema na wanyenyekevu.


Na zaidi ya yote mudumu katika upendo ninyi kwa ninyi, maana upendo unafunika zambi nyingi.


undugu juu ya kushikamana na ibada, na upendo juu ya undugu wenu.


Wapendwa wangu, ikiwa Mungu alitupenda sisi namna ile, sisi vilevile tunapaswa kupendana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ