Wanajibebesha sanamu hiyo juu ya mabega na kuipeleka, kisha wanaiweka pahali pake, nayo inakaa palepale; haiwezi hata kidogo kusogea kutoka pale inapokuwa. Mutu akiililia, haiwezi kumwitikia, wala haiwezi kumwokoa mutu katika taabu zake.
Sanamu zao ni kama sanamu za kutishia ndege katika shamba la maboga, hazina uwezo wa kuongea; ni lazima zibebwe maana haziwezi kutembea. Musiziogope sanamu hizo, maana haziwezi kuzuru, wala haziwezi kutenda jambo lolote jema.
Na wamoja kati yenu walikuwa kama wao. Lakini mumesafishwa toka zambi, mumetakaswa na kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.
Wao wenyewe wanaeleza namna mulivyotupokea wakati tulipofika kwenu na namna mulivyoacha kuabudu sanamu na kumurudilia Mungu. Mulifanya vile kusudi mumutumikie Mungu mwenye uzima na wa kweli
Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.
Kwa maana munajua namna gani mulivyokombolewa toka katika tabia za ovyo ovyo mulizoambukizwa na babu zenu. Hamukukombolewa kwa njia ya vitu vinavyoharibika kama vile feza au zahabu.
Kufuatana na hiyo, zamani mulipitisha siku nyingi mukifanya matendo yanayolingana na ya wapagani. Mulizoea kuishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, za ulevi na kuabudu sanamu.