Basi, ninyi hamuna nyumba munamoweza kukulia na kukunywea? Au munazarau kanisa la Mungu na munataka kuwapatisha haya wale wasiokuwa na kitu? Munataka niwaambie ninyi nini? Inafaa niwasifu? Hapana, siwezi kuwasifu hata kidogo juu ya jambo hilo!
Ni kwa sababu hii ninawatumia ninyi Timoteo. Yeye ni mwana wangu mupendwa na mwaminifu mbele ya Bwana. Atawakumbusha kanuni ninazofuata katika maisha yangu na Yesu Kristo, nami ninazofundisha fasi zote katika makanisa yote.
Kwa ngambo ingine, kila mutu aendelee kuishi kufuatana na zawadi aliyopewa na Bwana na kufuatana na vile alivyokuwa mbele ya kuitwa na Mungu. Hii ndiyo kanuni ninayofundisha katika makanisa yote.
Lakini sasa Timoteo amefika kwetu, akirudia toka kule kwenu. Ametuletea habari nzuri juu ya imani yenu na upendo wenu. Ametuelezea kwamba munatukumbuka vizuri siku zote, na kwamba muko na hamu sana ya kutuona, kama vile sisi nasi tunavyokuwa na hamu ya kuwaona.