9 Vilevile tusimupime Bwana kama vile wamoja wao walivyofanya, hata wakauawa na nyoka.
Walipatwa na tamaa kubwa kule katika jangwa, wakamupima Mungu kule kwenye ukiwa.
Walimujaribu Mungu kwa makusudi; wakidai wapewe chakula walichotaka.
Hata hivyo walimupima na kumwasi Mungu Mukubwa; wala hawakushika maagizo yake.
babu zenu waliponijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.
Kwa hiyo watu wakamunungunikia Musa wakisema: “Utupatie maji ya kunywa.” Musa akawauliza: “Mbona munaninungunikia? Mbona munamujaribu Yawe?”
Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”
“Musimujaribu Yawe, Mungu wenu, kama vile mulivyomujaribu huko Masa.