Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Ni yeye atakayewasimamisha ninyi imara mpaka mwisho kusudi musishitakiwe juu ya kosa lolote Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 1:8
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana nguvu za waovu zitavunjwa, lakini Yawe atawaimarisha watu wa haki.


maana Yawe anapenda haki, wala hawaachi waaminifu wake. Anawalinda hata milele; lakini wazao wa waovu wataangamizwa.


Kwa maana kama vile umeme unavyoangaza na kuonekana wazi katika mbingu yote, ni vile Mwana wa Mutu atakavyoonekana siku atakapokuja.


Ni hivi itakavyokuwa siku ile Mwana wa Mutu atakayotokea.


Wewe ni nani unayehukumu mutumishi wa mwingine? Akisimama imara katika kazi yake au akianguka, hilo ni shauri la bwana wake. Naye atasimama imara maana Bwana yuko na uwezo wa kumusimamisha.


Mungu asifiwe! Yeye yuko na uwezo wa kuwaimarisha katika imani juu ya Habari Njema ninayotangaza kwa kuhubiri ujumbe juu ya Yesu Kristo, kufuatana na ufunuo wa siri iliyofichwa tangia zamani za kale na kale.


Viumbe vyote vinangojea kwa hamu sana wakati Mungu atakapowaonyesha watoto wake waziwazi.


Lakini hali ya kazi ya kila mutu itaonekana wazi, kwa sababu Siku ile ya hukumu itaionyesha waziwazi. Kwa maana Siku ile itajitokeza katikati ya moto, na moto ule ndio utakaopima na kuonyesha hali ya kazi ya kila mutu.


Basi munapaswa kumutoa mutu yule kwa Shetani, kusudi mwili wake uharibiwe, nayo roho yake iweze kuokolewa Siku ile Bwana Yesu atakaporudi.


Basi katika barua zetu tunawaandikia tu mambo yale munayoweza kusoma na kufahamu. Ninatumaini kwamba mutafahamu mambo haya kabisa,


maana munayafahamu sasa kwa sehemu tu. Kwa Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu mutaweza kujivuna kwa ajili yetu kama vile tutakavyojivuna kwa ajili yenu.


Ni Mungu mwenyewe ndiye anayetuimarisha pamoja nanyi katika ushirika na Kristo, na ni yeye mwenyewe ndiye aliyetuchagua.


Alitaka hivi kujipatia yeye mwenyewe kanisa tukufu na takatifu, lisilokuwa na taka wala kikunjo wala kilema chochote.


kusudi mupate kutambua mambo yanayokuwa bora zaidi. Kwa hivi mutakuwa safi pasipo kosa kwa Siku ile ya kurudia kwa Kristo.


Ninajua hakika kwamba Mungu aliyeanza kazi hii njema ndani yenu, ataitimiza mpaka siku ile ya kurudi kwa Yesu Kristo.


Sasa, Mungu amewapatanisha ninyi naye, kwa njia ya kufa kwa Mwana wake kimwili, kusudi awawezeshe kuonekana mbele yake mukiwa watakatifu, bila kilema wala kosa lolote.


Mukuwe na mizizi ndani yake, mujijenge juu yake na kusimama imara katika imani sawa vile mulivyofundishwa. Na zaidi ya hii mukuwe wenye kushukuru sana.


Vilevile aitie mioyo yenu nguvu nanyi mutapata kuwa watakatifu na bila kosa mbele ya Mungu Baba yetu siku Bwana wetu Yesu atakaporudia pamoja na watakatifu wake wote.


Kwa maana munajua ninyi wenyewe kwamba siku Bwana atakaporudia, itatimia kwa saa musiyozania kama vile mwizi anavyokuja usiku.


musifazaike upesi wala kuogopa kwamba Siku ya kurudi kwa Bwana imekwisha kutimia. Inawezekana munafahamu mambo yale kwa njia ya unabii, mahubiri na barua inayosemeka kwamba imetoka kwetu.


Lakini Bwana ni mwaminifu, atawaimarisha na kuwakinga na yule Mwovu.


na kwa sababu hiyo ninapata mateso haya. Lakini sisikii haya kwa ajili ya ile. Maana ninajua ni nani yule niliyemwamini, nami ninahakikisha kwamba anaweza kuchunga kile alichonipa kwa kunilinda mpaka Siku ile ya kurudi kwake.


Bwana amusikilie huruma kwa Siku ile! Unajua vizuri sana vilevile mambo yote aliyonitendea kule Efeso.


Lakini mukisha kuteswa kwa muda kidogo, Mungu mwenye neema yote aliyewaita kusudi mupate kushiriki naye katika utukufu wake wa milele katika kuungana kwenu na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisha. Atawatia nguvu na kuwasimamisha imara kabisa.


Siku Bwana atakaporudi, itatimia kama vile mwizi anavyokuja. Siku ile mbingu zitatoweka kwa shindo kubwa, na viumbe vyote vinavyoangaza katika mbingu vitayeyuka. Dunia na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake vitateketezwa.


Kwa sababu hiyo, wapendwa wangu, mukiwa munangojea mambo yale, mufanye bidii apate kuwakuta safi bila kosa lolote na mukae na amani pamoja naye.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ