Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 hata hamukosewi zawadi yoyote ya Mungu, mukiwa mukingojea wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakapoonekana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 1:7
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Halafu kwa wakati ule, Ufalme wa mbinguni utafanana na wabinti kumi waliotwaa taa zao na kwenda kumupokea bwana-arusi.


Mukuwe kama watumishi wanaomungojea bwana wao arudie kutoka katika karamu ya ndoa, kusudi wakati anapofika na kupiga hodi wamufungulie mulango mara moja.


Ni hivi itakavyokuwa siku ile Mwana wa Mutu atakayotokea.


Viumbe vyote vinangojea kwa hamu sana wakati Mungu atakapowaonyesha watoto wake waziwazi.


Na si viumbe hivi tu; hata sisi tuliokwisha kuwa na Roho wa Mungu kama sehemu ya kwanza ya zawadi Mungu atakazotoa, tunaugua vilevile ndani yetu, tukingojea kukubaliwa na Mungu kuwa watoto wake, maana yake kukombolewa kwa kimwili.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Mumepungukiwa na nini kuliko makanisa mengine, isipokuwa tu kwamba mimi sikuwalemea kwa kupata musaada toka kwenu? Munisamehe kwa kosa hili.


Lakini sisi tunangojea kwa matumaini kwamba kwa uwezo wa Roho, tutahesabiwa haki kwa njia ya imani.


Lakini sisi ni wenyeji wa mbingu, tunamungojea Mwokozi wetu Bwana Yesu Kristo, afike kutoka kule.


Kristo ndiye uzima wenu wa kweli, naye atakapoonekana tena, basi ninyi mutaonekana pamoja naye katika utukufu wake.


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


na kuwapumzisha ninyi munaoteswa pamoja nasi. Jambo lile litatendeka wakati Bwana Yesu atakapoonekana tokea mbinguni pamoja na wamalaika wake wenye uwezo,


Tangia sasa nimetayarishiwa zawadi ya ushindi, ndiyo ile taji ya haki, ambayo Bwana anayekuwa Mwamuzi wa haki atakayonipa siku ile ya kurudi kwake. Wala hatanipa mimi peke yangu tu, lakini na wale wote wanaopenda kumwona wakati atakaporudi.


Na hivi tutaishi tukingojea ule uheri tunaoutumainia, wakati utukufu wa Mungu wetu Mukubwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo utakapotokea.


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


Kwa sababu hiyo, mukuwe tayari kwa kutumikisha akili yenu. Mukeshe na muweke tumaini lenu lote katika baraka ile mutakayopewa wakati Yesu atakapotokea.


Lakini mufurahi kwa sababu munashiriki katika mateso ya Kristo. Na kwa hiyo mutashangilia kwa furaha wakati atakapoonekana katika utukufu.


Na wakati Muchungaji Mukubwa atakapotokea, mutapokea taji ya utukufu isiyoweza kuharibika.


mukingojea na kuharikisha kuja kwa Siku ile ya Mungu; ndiyo siku mbingu zitakapoyeyushwa kwa moto, na viumbe vyote vinavyoangaza katika mbingu vitakapoyeyuka.


Wapendwa wangu, sasa sisi ni watoto wa Mungu, wala namna tutakavyokuwa haijaonekana bado waziwazi. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwa sababu tutamwona vile anavyokuwa.


Mudumu katika upendo wa Mungu, mukimungojea Bwana wetu Yesu Kristo, atakayewapa ninyi uzima wa milele kwa huruma yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ