Wakubwa wa muji wa Soani ni wapumbafu kabisa, washauri wa Mufalme wa Misri wanatoa shauri la kijinga! Kila mumoja anaweza namna gani kumwambia Mufalme wa Misri: Mimi ni wa uzao wa wenye hekima, wa uzao wa wafalme wa zamani!
Hivyo, nitawatendea tena watu hawa maajabu, mambo ya ajabu na ya kushangaza. Nao wenye hekima wao wataishiwa hekima, na akili ya wenye akili wao itatoweka.
Nani asiyekuogopa wewe, ee mufalme wa mataifa? Wewe unastahili kuheshimiwa: kwa maana kati ya wenye hekima wote wa mataifa, na katika falme zao zote, hakuna hata mumoja anayekuwa kama wewe.
Kwa maana hekima ya kidunia ni upumbafu mbele ya Mungu. Ni sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mungu anawanasa wenye hekima katika werevu wao wenyewe.”
Sisi ni wapumbafu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika kuungana kwenu na Kristo. Sisi ni zaifu, lakini ninyi ni wenye nguvu. Tunazarauliwa, lakini ninyi munaheshimiwa!
Wandugu zangu, nimesema maneno haya nikitwaa mufano wa Apolo na wangu mimi mwenyewe kusudi yakuwe fundisho kwenu. Nilitaka kwamba kufuatana na mufano huu mujifunze maana ya masemi haya: “Musipite pembeni ya maandiko.” Hata mutu mumoja kati yenu asijivunie mutu fulani na kuzarau mwingine.