Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Ninataka kusema: kila mumoja kati yenu anasema maneno yake mbalimbali. Mumoja anasema: “Mimi ni wa Paulo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Petro,” na mwingine anasema: “Mimi ni wa Kristo.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 1:12
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa, watu wa Israeli waligawanyika kwa makundi mawili: kundi moja lilimutambua Tibuni mwana wa Ginati kuwa mufalme, na kundi la pili lilimutambua Omuri.


Lakini ninyi musikubali kuitwa ‘Mwalimu’, kwa maana ninyi wote ni wandugu, nanyi muko na Mwalimu mumoja tu.


Kisha akamupeleka Simoni kwa Yesu. Yesu akamwangalia, akasema: “Wewe ndiwe Simoni mwana wa Yoane, sasa utaitwa Kefa.” (Jina “Kefa” ni sawasawa na “Petro” na maana yake ni “Jiwe.”)


Katika siku zile, Muyuda mumoja, jina lake Apolo, muzaliwa wa muji Alesanduria, alikuwa amefika katika muji Efeso. Alikuwa mutu mwenye uwezo katika masemi na mwenye kuelewa sana Maandiko.


Wakati Apolo alipokuwa Korinto, Paulo akasafiri akipitia katika inchi ya vilima na kufika Efeso. Kule akakuta wanafunzi wamoja;


Kwa maana, wandugu zangu, nimepata habari zenu kwa njia ya jamaa ya Kloe kwamba kuko ugomvi katikati yenu.


Alimutokea Petro, na kisha akawatokea mitume wake kumi na wawili.


Wandugu zangu, muangalie, jambo ninalotaka kusema ni hili: kile kilichoumbwa kwa nyama na damu hakiwezi kupata urizi katika Ufalme wa Mungu katika hali ile, wala hakuna chenye hali ya kuharibika kinachoweza kuwa na hali ya kutoharibika.


Kwa ngambo ya ndugu yetu Apolo, nimemusihi sana akuje kwenu pamoja na wandugu wengine, lakini hakutaka kabisa kwenda sasa; atakwenda kwa wakati utakaomupendeza.


Wandugu zangu, nimesema maneno haya nikitwaa mufano wa Apolo na wangu mimi mwenyewe kusudi yakuwe fundisho kwenu. Nilitaka kwamba kufuatana na mufano huu mujifunze maana ya masemi haya: “Musipite pembeni ya maandiko.” Hata mutu mumoja kati yenu asijivunie mutu fulani na kuzarau mwingine.


Wandugu zangu, mimi ninataka kusema hivi: wakati uliopangwa unabaki mufupi. Tangu sasa wale waliooa waishi kama vile wasiooa.


Au sina haki ya kusafiri pamoja na mwanamuke mukristo kama vile mitume wengine wanavyofanya, nao wandugu za Bwana na hata Petro?


Ninyi munaangalia tu namna vitu vinavyoonekana kwa inje. Mutu yeyote anayejiaminia kwamba yeye ni wa Kristo, inafaa afikiri tena yeye mwenyewe mambo haya: ikiwa yeye ni wa Kristo sisi vilevile ni wa Kristo.


Mukumbuke maneno haya: yule anayepanda kidogo atavuna kidogo, na yule anayepanda kwa uwingi atavuna kwa uwingi.


Basi Yakobo, Petro na Yoane, waliohesabiwa kuwa waongozi wakubwa, walitambua neema ile niliyojaliwa na Mungu wakatupatia mukono, mimi na Barnaba kuwa kitambulisho cha ushirika. Hivi tukapatana kwamba sisi tutakwenda kuhubiri watu wa mataifa mengine na wao watakwenda kuhubiri Wayuda.


Mambo ninayotaka kusema ni haya: Mungu amekwisha kufanya agano kwa njia ya haki. Nayo Sheria iliyotokea miaka mia ine makumi tatu nyuma yake haiwezi kulivunja au kugeuza ile ahadi ya Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ