Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 9:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Watu wengine watajibu: ‘Ni kwa sababu walimwacha Yawe, Mungu wao, aliyewatoa babu zao katika inchi ya Misri, wakashikamana na miungu mingine, wakaiabudu na kuitumikia; kwa hiyo, Yawe amewaletea hasara hizi zote.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 9:9
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Elia akamujibu: “Mwenye kutaabisha Waisraeli si mimi, lakini ni wewe na jamaa ya baba yako. Ninyi mumepita pembeni ya amri za Yawe na kuabudu Bali.


Kwa sababu wameniacha na kufukizia miungu mingine ubani kusudi watu wanikasirikishe kwa kazi zote za mikono yao, basi, kasirani yangu juu ya Yerusalema itawaka na haitaweza kutulizwa.


Kwa sababu hii, Yawe akakasirikia sana inchi ya Yuda na Yerusalema, na yale aliyowatendea yalikuwa ya kushangaza, ya kuogopesha na ya kuchekelewa. Haya yote mumeyaona wenyewe kwa macho yenu.


Watu wengine watajibu: ‘Ni kwa sababu walimwacha Yawe, Mungu wa babu zao aliyewatoa toka katika inchi ya Misri; wakashikamana na miungu mingine, wakaiabudu na kuitumikia. Kwa hiyo Yawe amewaletea hasara hizi zote.’ ”


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Na watu wengi wa mataifa watapita karibu na muji huu, kila mumoja atamwuliza mwenzake: Kwa nini Yawe ameutendea muji huu mukubwa hivi?


Hasara hizi zimewapata mpaka leo kwa sababu muliitolea miungu mingine sadaka za kuteketezwa na kumukosea Yawe, mukakataa kusikiliza sauti yake au kufuata sheria yake, masharti yake na maagizo yake.


Na watu wenu watakapouliza: Kwa nini Yawe, Mungu wetu, ametutendea mambo hayo yote? Wewe Yeremia utawajibu hivi: Ninyi mulimwacha Yawe, mukaitumikia miungu ya kigeni katika inchi yenu. Basi ndivyo mutakavyowatumikia watu wengine katika inchi isiyokuwa yenu.


Watu wote waliowakuta waliwaua, na waadui zao wamesema: Sisi hatuna kosa, maana hao wamemukosea Yawe anayekuwa makao yao ya kweli; Yawe ambaye ni tegemeo la babu zao!


Wapita njia wote wanakuchekelea; wanakupigia muunzi, ee Yerusalema, wakitikisa vichwa vyao kwa mazarau na kusema: Huu ndio ule muji uliofikia ukamilifu wa uzuri, muji uliokuwa furaha ya dunia nzima?


Hata mataifa yote yatasema: ‘Kwa nini Yawe ameitendea hivyo inchi hii? Hasira hii kubwa ina maana gani?’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ