Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 9:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Nawe kama ukinitumikia kwa ukamilifu wa moyo na usawa kama baba yako Daudi alivyofanya, ukitii amri zangu na kutimiza yale yote niliyokuamuru, ukifuata masharti yangu na maagizo yangu,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 9:4
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


Si ni Abrahamu mwenyewe ndiye aliyesema kwamba huyu ni dada yake? Tena hata Sara mwenyewe alisema kwamba Abrahamu ni kaka yake! Mimi nimefanya nilivyofanya kwa moyo safi na sina kosa.”


Maana nimefuata njia za Yawe, wala sikujitenga na Mungu wangu kwa ajili ya uovu.


Na kama utashika yote nitakayokuamuru, kama utaishi kulingana na mapenzi yangu, kama utatenda mema mbele yangu kwa kushika masharti yangu na amri zangu, kama vile mutumishi wangu Daudi alivyofanya, mimi nitakuwa pamoja nawe siku zote. Na nitakupatia inchi ya Israeli na kuufanya utawala wako ukuwe imara kama nilivyomufanyia Daudi.


Maana, alipokuwa muzee, wake zake walimupotosha hata akaitumikia miungu mingine, wala hakukuwa mwaminifu kabisa kwa Yawe, Mungu wake, kama baba yake Daudi alivyokuwa mwaminifu.


Hivyo, Solomono alitenda maovu mbele ya Yawe, wala hakufuata kwa ukamilifu mapenzi ya Yawe kama baba yake Daudi alivyokuwa amefanya.


nikaunyanganya ufalme utoke kwa wazao wa Daudi, nikakupa wewe. Lakini wewe ni kinyume kabisa cha mutumishi wangu Daudi ambaye alizishika amri zangu. Alifuata mapenzi yangu kwa moyo wake wote na kutenda tu yanayokuwa sawa mbele ya macho yangu.


Yawe alifanya hivyo kwa sababu Daudi alitenda mema mbele yake na hakuenda pembeni ya maagizo ya Yawe siku za maisha yake yote, isipokuwa tu lile jambo la Uria Muhiti.


Tena kama ukifuata njia yangu na kushika masharti na amri zangu kama vile baba yako Daudi alivyofanya, basi, nitakupa maisha marefu.”


Solomono alimupenda Yawe, akashika masharti ya baba yake Daudi; lakini tu, naye alitoa sadaka na kufukiza ubani juu ya vilima.


Solomono akamwambia: “Ulimwonyesha wema mwingi mutumishi wako Daudi, baba yangu, kwa sababu alikutumikia kwa uaminifu, kwa haki na kwa moyo wa usawa; na umedumisha mema yako kwa kumupa mwana anayeikaa sasa kwenye kiti chake cha kifalme.


“Juu ya nyumba hii unayoijenga, kama ukifuata masharti yangu, ukiyatii maagizo yangu na amri zangu zote, nitakutimizia mambo yote niliyomwahidi baba yako Daudi.


Kwa hiyo, sasa, ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba vilevile utimize ile ahadi uliyomwahidi mutumishi wako Daudi, baba yangu, ukisema: ‘Siku zote utakuwa na mutu mumoja wa uzao wako kwa kuikaa katika kiti cha kifalme cha Israeli, ikiwa wazao wako watakuwa waangalifu juu ya mwenendo wao mbele yangu kama wewe ulivyofanya mbele yangu.’


“Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote na kutenda mazuri mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.


Yeye alimutafuta Mungu wa babu yake na kutii amri zake, wala hakufuata matendo ya Israeli.


Nitashikamana na mwenendo mukamilifu. Utakuja kwangu wakati gani? Nitaishi kwa ukamilifu ndani ya nyumba yangu;


Wimbo wa safari za kidini. Heri wote wanaomwabudu Yawe, wanaoishi kufuatana na amri zake.


Ni mutu anayefanya hivi: anaishi katika ukamilifu, anatenda kwa haki siku zote, anasema ukweli kutoka ndani ya moyo, hatetani, hatendei rafiki yake uovu, hamutukani jirani yake, anazarau wapotevu, anaheshimu wanaomwabudu Yawe, hageuzi kiapo chake hata kikimuletea hasara, hakopeshi feza yake kwa kupata faida, wala kupokea kituliro kumutesa asiyekuwa na kosa. Mutu anayefanya vile, hatatikisika hata kidogo.


Zaburi ya Daudi. Ee Yawe, unitetee, maana nimeishi katika ukamilifu, nimekutumainia wewe bila kusita.


Lakini mimi ninaishi katika ukamilifu; unihurumie na kunikomboa.


Daudi akawafundisha kwa moyo mukamilifu, akawaongoza kwa uhodari mukubwa.


Anayeishi kwa ukamilifu anaishi salama, lakini anayepotosha maisha yake atagunduliwa.


Heri watoto wa mutu wa haki mwenye mwenendo mukamilifu!


Mwenye mwenendo mukamilifu ataponyeshwa, lakini munafiki wa njia mbili ataanguka mara moja.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Ukifuata njia zangu na kushika maagizo niliyokupa, basi, utaisimamia nyumba yangu na viwanja vyake. Nami nitakuwezesha kuingia katika utumishi wangu kama hawa wanaosimama mbele yangu.


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


“Kama mukiitii sauti ya Yawe, Mungu wenu, na kushika kwa uangalifu amri ambazo ninawaamuru leo, yeye atawaweka juu ya mataifa yote katika dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ