1 Wafalme 9:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20024 Nawe kama ukinitumikia kwa ukamilifu wa moyo na usawa kama baba yako Daudi alivyofanya, ukitii amri zangu na kutimiza yale yote niliyokuamuru, ukifuata masharti yangu na maagizo yangu, အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Na kama utashika yote nitakayokuamuru, kama utaishi kulingana na mapenzi yangu, kama utatenda mema mbele yangu kwa kushika masharti yangu na amri zangu, kama vile mutumishi wangu Daudi alivyofanya, mimi nitakuwa pamoja nawe siku zote. Na nitakupatia inchi ya Israeli na kuufanya utawala wako ukuwe imara kama nilivyomufanyia Daudi.
Kwa hiyo, sasa, ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba vilevile utimize ile ahadi uliyomwahidi mutumishi wako Daudi, baba yangu, ukisema: ‘Siku zote utakuwa na mutu mumoja wa uzao wako kwa kuikaa katika kiti cha kifalme cha Israeli, ikiwa wazao wako watakuwa waangalifu juu ya mwenendo wao mbele yangu kama wewe ulivyofanya mbele yangu.’
Ni mutu anayefanya hivi: anaishi katika ukamilifu, anatenda kwa haki siku zote, anasema ukweli kutoka ndani ya moyo, hatetani, hatendei rafiki yake uovu, hamutukani jirani yake, anazarau wapotevu, anaheshimu wanaomwabudu Yawe, hageuzi kiapo chake hata kikimuletea hasara, hakopeshi feza yake kwa kupata faida, wala kupokea kituliro kumutesa asiyekuwa na kosa. Mutu anayefanya vile, hatatikisika hata kidogo.