Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 9:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yawe alimwambia: “Nimesikiliza wakati uliponiomba na kunisihi. Nimeitakasa nyumba hii ambayo umenijengea kusudi watu waabudu jina langu hapa milele. Nitaichunga na kuipenda wakati wote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 9:3
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uchunge nyumba hii usiku na muchana, nafasi ambapo umesema: ‘Hapo ndipo watu watakapoliheshimu jina langu’. Unisikilize ninapokuja pahali hapa kwa kuomba.


“Rudi umwambie Hezekia, mukubwa wa watu wa Yawe, na kumwambia: Mimi, Yawe, Mungu wa babu yako Daudi, nimesikia ombi lako na nimeona machozi yako. Nitakuponyesha na nyuma ya siku tatu utaenda katika nyumba ya Yawe.


Nayo sanamu ya Ashera aliyotengeneza akaiweka katika nyumba ambayo Yawe alisema juu yake mbele ya Daudi na mwana wake Solomono: “Katika nyumba hii na katika Yerusalema niliouchagua ndipo pahali nitakapoabudiwa milele.


Nayo sanamu aliyotengeneza, akaiweka katika nyumba ya Mungu ambayo aliizungumuzia, mbele ya Daudi na mwana wake Solomono: “Katika nyumba hii na katika Yerusalema kati ya makabila kumi na mawili ya Israeli, ndipo pahali nitakapoabudiwa milele.


“Sasa ee Mungu wangu, utuangalie na upokee maombi tutakayoomba pahali hapa.


Mungu aliyeuchagua Yerusalema kuwa pahali pake pa kuabudiwa amwangushe mufalme au taifa lolote litakalopinga amri hii au kutaka kuiharibu nyumba hii ya Mungu inayokuwa katika Yerusalema. Ni mimi Dario niliyetoa amri hii na inapaswa kushikwa.


Ee Yawe, unapokea maombi ya muzaifu; unamutia moyo na kumutegea sikio.


Ninamupenda Yawe, kwa maana ananisikia, maana amesikia kilio cha ombi langu.


lakini anawapinga watu wanaotenda maovu, kusudi afute majina yao kutoka katika dunia.


maana wewe unajibu maombi yetu. Wanadamu wote watakuja kwako wewe peke.


Lakini kweli Mungu amenisikiliza; amesikiliza maneno ya maombi yangu.


Maana kwa siku sita mimi Yawe niliumba mbingu na inchi, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, kisha nikapumzika siku ya saba. Kwa hiyo mimi Yawe nilibariki siku ya Sabato, nikaitakasa.


Hema la mukutano na mazabahu nitavifanya vitakatifu. Vilevile Haruni na wana wake nitawatakasa kusudi wanitumikie kama makuhani.


Kisha Yawe akaniambia: Hata kama Musa na Samweli wangesimama mbele yangu na kunisihi, singewahurumia watu hawa. Uwaondoe kabisa mbele yangu. Uwaache waende!


Kisha, mutakuja na kusimama mbele yangu katika hekalu hili linalojulikana kwa jina langu na kusema “Tuko salama”, ingawa munaendelea kufanya mambo hayo yanayonichukiza.


Ulipoanza kuomba, Mungu alitoa jibu, nami nimekuja kukuelezea jibu hilo kwa sababu unapendwa sana. Kwa hiyo, usikilize kwa uangalifu jibu hilo na kuelewa maono hayo.


Basi muangalie namna munavyopaswa kusema munapoomba: ‘Baba yetu unayekuwa mbinguni, Jina lako litukuzwe;


Na ninajua kwamba unanisikia siku zote, lakini ninasema hivi kwa sababu ya watu hawa wanaokusanyika hapa kusudi wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”


Naye akaniambia: ‘Kornelio, Mungu amesikia maombi yako na kukukumbuka kwa ajili ya misaada unayotoa kwa wamasikini.


inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anatunza. Siku zote anaiangalia tangu mwanzo wa mwaka hata mwisho wa mwaka.


basi huko pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kusudi jina lake likae pale, hapo mutapeleka yote ninayowaamuru: sadaka zenu za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, na sadaka za kutimiza kiapo.


Basi, pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua, apaweke jina lake, hapo munaweza kuchinja ngombe au kondoo yeyote ambaye Yawe amewajalia, kama nilivyowaamuru na munaweza kula kiasi chochote munachotaka cha nyama hiyo, kama mukiwa katika miji yenu.


Lakini mutakwenda pahali ambapo Yawe, Mungu wenu, atachagua katika makabila yote kwa kuweka jina lake na makao yake hapo. Huko ndiko mutakakokwenda.


Mutafurahia mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi pamoja nanyi. Mufanye haya katika pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kwa ajili ya jina lake.


Nasi tuko na tumaini hili mbele ya Mungu: tunajua kwamba atatusikiliza tukimwomba kitu chochote kufuatana na mapenzi yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ