Solomono alifanya mapatano na mufalme wa Misri, kwa kumwoa binti yake. Akamuleta binti wa mufalme wa Misri na kumuweka katika muji wa Daudi, mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake mwenyewe, nyumba ya Yawe, na ukuta wa kuuzunguka Yerusalema.
Na katika mwezi wa Buli, ni kusema mwezi wa nane, katika mwaka wa kumi na mumoja, ujenzi wa nyumba ulimalizika, na kazi ilikuwa imekamilika kama ilivyopangwa. Solomono alitumia miaka saba kwa kujenga.
mufalme Solomono alimupa Hiramu mufalme wa Tiro miji makumi mbili katika jimbo la Galilaya kwa sababu yule Hiramu alikuwa amemupelekea Solomono mbao za mierezi na miberoshi, na zahabu vilevile, kadiri alivyohitaji kwa majengo.
Wao wakatujibu hivi: “Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na dunia, na tunaijenga upya nyumba ambayo ilikuwa imejengwa na kumalizika pale mbele na mufalme mumoja mukubwa wa Israeli.”