Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 9:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Mufalme Solomono alipomaliza kujenga nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme na majengo mengine yote aliyokusudia kujenga,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 9:1
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Solomono alifanya mapatano na mufalme wa Misri, kwa kumwoa binti yake. Akamuleta binti wa mufalme wa Misri na kumuweka katika muji wa Daudi, mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake mwenyewe, nyumba ya Yawe, na ukuta wa kuuzunguka Yerusalema.


Musingi wa nyumba ya Yawe ulijengwa katika mwezi wa Zivu, katika mwaka wa ine.


Solomono alijijengea nyumba ya kifalme, naye alitumia muda wa miaka kumi na mitatu kwa kuimaliza.


Kisha, akajenga jengo lililoitwa Nyumba ya pori ya Lebanoni. Urefu wake ulikuwa metre makumi ine na ine na nusu, upana wake metre makumi mbili na mbili na sentimetre makumi mbili na tano, na urefu wake wa kwenda juu metre kumi na tatu na nusu. Ilikuwa imejengwa juu ya mistari mitatu ya nguzo za mierezi, nguzo ambazo zilishikilia boriti za mierezi kwa upande wa juu.


Basi, mufalme Solomono akamaliza kazi zote zilizoelekea nyumba ya Yawe. Kisha Solomono akaleta mali yote ambayo baba yake Daudi, alikuwa ameitoa kwa Bwana, ni kusema: feza, zahabu na vyombo; akaiweka katika hazina za nyumba ya Yawe.


Katika siku ya nane, Solomono aliwaaga watu; nao wakamutakia mufalme baraka, wakaenda kwao wakishangilia na kufurahi kwa sababu ya wema ambao Yawe aliuonyesha kwa Daudi, mutumishi wake, na kwa watu wake Waisraeli.


Kisha miaka makumi mbili ambayo Solomono alipitisha kwa kuzijenga nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme,


mufalme Solomono alimupa Hiramu mufalme wa Tiro miji makumi mbili katika jimbo la Galilaya kwa sababu yule Hiramu alikuwa amemupelekea Solomono mbao za mierezi na miberoshi, na zahabu vilevile, kadiri alivyohitaji kwa majengo.


na miji yake yote ya kuwekea akiba, magari yake ya vita, na waaskari wapanda-farasi wake; vilevile na chochote alichotaka kujenga katika Yerusalema, Lebanoni au nafasi ingine katika ufalme wake.


Solomono alipomaliza maombi yake, moto ukashuka kutoka mbinguni na kuchoma sadaka na sadaka za kuteketeza kwa moto zilizotolewa, kisha utukufu wa Yawe ukajaza nyumba.


Basi, mufalme Solomono akamaliza kujenga nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme na kutimiza yale yote aliyokusudia kuifanyia nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme.


Kisha miaka makumi mbili, ambayo Solomono alipitisha kwa kujenga nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme,


muji wa Balati, na miji yake yote ya kuwekea magari yake ya vita na ya waaskari wapanda-farasi wake, na kitu chochote alichotaka kujenga katika Yerusalema, Lebanoni au nafasi ingine katika ufalme wake.


Kila kitu macho yangu yalichokitamani nilikipata. Moyo wangu sikuunyima raha yoyote. Moyo wangu ulifurahia mambo niliyotenda, na hii ilikuwa zawadi ya jasho langu.


Nilifanya mambo makubwa: nilijenga nyumba na kujilimia mashamba ya mizabibu.


Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kumata upepo. Afazali kufurahia kitu ambacho uko nacho kuliko kuhangaika kwa kutamani kitu kingine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ