Sanamu hizo zilielekeana, zikiwa na mabawa yaliyokunjuliwa: bawa la mumoja likigusa ukuta mumoja, na bawa la mwingine likigusa ukuta wa pili, na yale mengine yaligusana katikati ya chumba.
Kisha makuhani wakaliingiza Sanduku la Agano la Yawe kwa nafasi yake katika chumba cha ndani cha nyumba, ni kusema Pahali Patakatifu Sana, chini ya mabawa ya makerubi.
Kwa sababu miti hiyo ilikuwa mirefu sana, incha zake ziliweza kuonekana kutoka Pahali Patakatifu, mbele ya chumba cha ndani; lakini haikuweza kuonekana kutoka upande wa inje. Miti hiyo ingali pahali pale hata leo.
Juu yake wataweka kifuniko cha ngozi laini ya mbuzi, kisha watatandaza juu yake kitambaa cha rangi ya samawi tupu. Halafu wataingiza miti ya kulibebea sanduku hilo.
Na juu ya lile sanduku kulikuwa sanamu mbili za makerubi zilizoonyesha utukufu wa Mungu. Mabawa yao yalikuwa yakinyooshwa juu ya kiti cha rehema. Lakini sasa si wakati wa kueleza mambo hayo yote moja kwa moja.