Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 8:57 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

57 Yawe, Mungu wetu, akuwe nasi kama alivyokuwa na babu zetu. Tunaomba asituachilie, wala asitutupilie.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 8:57
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”


Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika; Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka.


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure; mufanye mipango lakini haitawezekana, maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Hapo hasira yangu itawawakia siku hiyo, nami nitawaacha na kuficha uso wangu mbali nao, wataangamizwa. Maovu mengi na taabu zitawapata hata watambue kwamba maovu hayo yamewapata kwa sababu Mungu wao hayuko kati yao.


Mukuwe imara na hodari, wala musiwaogope au kutishwa nao, maana Yawe, Mungu wenu, ndiye anayekwenda pamoja nanyi. Yeye hataacha kuwasaidia na hatawatupa.”


Yawe ndiye anayewaongoza. Yeye atakuwa pamoja nanyi. Yeye hataacha kuwasaidia na hatawatupa. Hivyo, musiogope wala musifazaike.”


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


Hakuna mutu atakayekushinda siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Musa. Siku zote nitakuwa nawe wala sitakuacha hata kidogo.


Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”


Naye akawaambia: “Basi, muondoe miungu ya kigeni munayokuwa nayo, mumufuate Yawe, Mungu wa Israeli, kwa moyo wenu wote.”


Kwa heshima ya jina lake kubwa, Yawe hatawatupa watu wake kwa sababu amependa kuwafanya ninyi mukuwe watu wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ