Uchunge nyumba hii usiku na muchana, nafasi ambapo umesema: ‘Hapo ndipo watu watakapoliheshimu jina langu’. Unisikilize ninapokuja pahali hapa kwa kuomba.
Kwa sababu, ee Bwana wetu Yawe, uliwatenga na watu wa mataifa mengine katika dunia, kusudi wakuwe mali yako, kama ulivyotangaza kwa njia ya Musa, mutumishi wako, wakati ule ulipowatoa babu zetu katika inchi ya Misri.”