Mufalme Daudi aliposikia kwamba Yawe ameibariki jamaa ya Obedi-Edomu na vitu vyote alivyokuwa navyo kwa sababu ya Sanduku la Mungu, akaenda kuliondoa Sanduku la Agano kutoka katika nyumba ya Obedi-Edomu na kulipeleka kwenye muji wa Daudi kwa shangwe.
Wakati mumoja, Solomono alikwenda kutoa sadaka kule kwenye kilima cha Gibeoni, maana palikuwa ndipo pahali pakubwa pa ibada. Ilikuwa ni kawaida ya Solomono kutoa maelfu ya sadaka za kuteketezwa katika mazabahu hiyo.
Kisha akaandamana nao mpaka pahali pa ibada kule Gibeoni. Walikwenda kule kwa sababu pale ndipo pahali palipokuwa hema la mukutano la Mungu ambalo Musa mutumishi wa Yawe, alilotengeneza katika jangwa.