Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 8:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Basi, mufalme Solomono akawakusanya mbele yake kule Yerusalema wazee na viongozi wote wa makabila na wa ukoo za Waisraeli kusudi waliondoe Sanduku la Agano la Yawe katika muji wa Daudi, ni kusema Sayuni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 8:1
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walipofika kwenye uwanja wa kupepetea ngano wa Nakoni, Uza aliunyoosha mukono wake na kuligusa Sanduku la Mungu kwa sababu wale ngombe walijikwaa.


Solomono alipoamuka, alitambua kwamba ilikuwa ndoto. Halafu akarudi Yerusalema, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Yawe, akamutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Halafu akawafanyia watumishi wake wote karamu.


Daudi alikaa katika makimbilio yale, na kwa hiyo, muji ule ukaitwa “Muji wa Daudi.”


Basi, Daudi, wazee wa Waisraeli na majemadari wa maelfu, wakaenda kutwaa Sanduku la Agano la Yawe kutoka katika nyumba ya Obedi-Edomu kwa shangwe.


Sanduku la Agano la Yawe lilipokuwa likiingia katika muji wa Daudi, Mikali, binti wa Saulo, akachungulia kwenye dirisha, akamwona mufalme Daudi akicheza na kushangilia, basi akamuzarau ndani ya moyo wake.


Basi, akawakusanya Waisraeli wote wakuje Yerusalema, kwa kuleta Sanduku la Agano la Yawe pahali alipolitayarishia.


Mufalme Daudi akakusanya kule Yerusalema wakubwa wote wa Waisraeli: wa makabila, majemadari na vikundi waliomutumikia mufalme, wakubwa wa maelfu na mamia, wasimamizi wa mali yote, ya ngombe wote wa mufalme na wana wake pamoja na wakubwa wa nyumba ya kifalme, mashujaa na waaskari wenye heshima.


Mufalme Hezekia akawatumia ujumbe watu wote wa Israeli na Yuda, na vilevile akawaandikia barua watu wa kabila la Efuraimu na Manase, akiwaalika wote wakuje katika nyumba ya Yawe kule Yerusalema, kusudi wafanye sikukuu ya Pasaka kwa heshima ya Yawe, Mungu wa Israeli.


Wakati mwezi wa saba ulipofika, na watu wa Israeli wakiwa wamekwisha kukaa katika miji yao, wote wakakusanyika pamoja katika Yerusalema.


akasikia malalamiko ya wafungwa, akawaachilia huru waliohukumiwa kuuawa.


Wanaojua jina lako, wanakutegemea, kwa maana wewe, ee Yawe, hauwatupi wanaokutafuta.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.


Siku ya kuwakomboa inakaribia, haiko mbali tena; siku ya kuwaokoa ninyi haitachelewa. Nitauokoa Sayuni, nitaleta utukufu kwa Israeli.


Kiongozi mumoja wa jamaa kutoka kila kabila atakusaidia kufanya hesabu.


Yoshua aliwaita Waisraeli wote pamoja na viongozi na wazee wao, waamuzi na wakubwa, akawaambia: “Sasa mimi nimekuwa muzee wa miaka mingi.


Kisha Yoshua akayakusanya makabila yote ya Waisraeli kule Sekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na wakubwa wa Waisraeli, nao wakakuja mbele ya Mungu.


Kwa kuwa imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: “Nimesimika jiwe kubwa la pembe katika Sayuni, jiwe lile ni la bei kali. Ni mimi niliyelichagua. Yule anayelitumainia hatapata haya.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ