Kila mustari ulikuwa na nguzo kumi na tano; basi zote pamoja zilikuwa nguzo makumi ine na tano. Vyumba vilivyojengwa juu ya nguzo hizo, alivitilia dari ya mbao za mierezi.
Kulikuwa matundu madogomadogo kwenye miimo ya inje ya vyumba vyote na hata kwenye kuta zilizotenganisha vyumba. Kulikuwa michoro ya miti ya ngazi kwenye miimo ya ndani iliyoelekea baraza la kupitia.
Chumba cha kuingilia na madirisha na nguzo zake, pamoja na ile miti ya ngazi iliyochorwa juu ya ukuta, vyote vilifanana na vile vya mulango wa upande wa mashariki.
Kulikuwa madirisha pande zote kama ilivyokuwa katika vyumba vingine. Urefu wake ulikuwa metre makumi mbili na tano na upana wake metre kumi na mbili na nusu.
Vyumba vya walinzi, baraza, na kuta zake vilikuwa na ukubwa ule ule kama vile vingine; kulikuwa vilevile madirisha kandokando ya hiyo njia ya kuingilia na kwenye baraza. Ilikuwa na urefu metre makumi mbili na tano na upana metre kumi na mbili na nusu.
Vyumba vyake vya walinzi, nguzo zake za ndani pamoja na baraza vilikuwa na ukubwa kama vile vingine. Kulikuwa madirisha pande zote hata kwenye baraza na chumba cha kuingilia. Urefu wake ulikuwa metre makumi mbili na tano na upana wake metre kumi na mbili na nusu.
Huko nako kulikuwa vyumba vya walinzi, kuta za ndani zilizopambwa, baraza ya kuingilia na madirisha pande zote. Urefu wake wote ulikuwa metre makumi mbili na tano na upana metre kumi na mbili na nusu.