Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 7:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Hiramu alitengeneza birika la maji la muviringo lenye upana wa metre ine na nusu kutoka ukingo mpaka ukingo, na urefu wa metre mbili na sentimetre makumi mbili na muzunguko wa metre kumi na tatu na nusu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 7:23
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Vichwa vya nguzo hizo vilipambwa kwa mufano wa maua ya yungiyungi. Na hivyo kazi ya kutengeneza nguzo ikamalizika.


Kisha alimwamuru Uria: “Tumia hii mazabahu yangu kubwa kwa kuteketeza sadaka za asubui na sadaka za unga za magaribi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za unga za mufalme na za watu wote na vilevile sadaka za divai za watu. Unyunyize damu ya nyama wote wa kuteketezwa ambao wametolewa sadaka. Lakini ile mazabahu ya shaba nitaitumia mimi kwa kuuliza shauri toka kwa Mungu.”


Mufalme Ahazi aliviondoa vile vishikio vilivyokuwa vikisimamishwa kule, akaondoa na bakuli lake ambalo lilikuwa juu ya wale ngombe dume kumi na wawili wa shaba na kuliweka juu ya musingi wa mawe.


Wababeli walivunja vipandevipande nguzo za shaba ambazo zilikuwa katika nyumba ya Yawe, pamoja na viikalio vya birika kubwa la shaba nyeusi lililokuwa mule katika nyumba ya Yawe, wakapeleka shaba nyeusi mpaka Babeli.


Daudi alichukua vilevile shaba nyingi sana kutoka muji wa Tibuhati na muji wa Kuni iliyokuwa miji ya Hadadezeri. Solomono alitumia shaba hiyo kwa kutengeneza nguzo na vyombo vya shaba.


Kisha, akatengeneza birika la maji la muviringo, lenye upana wa metre ine na nusu kutoka ukingo mpaka ukingo, lenye urefu wa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano, na lenye muzunguko wa metre kumi na tatu na nusu.


Kisha akatengeneza birika la shaba na tako lake la shaba. Birika hilo lilitengenezwa kwa kutumia vioo vya shaba vya wanawake waliotumika kwenye mulango wa hema la mukutano.


Kwa maana Yawe wa majeshi anasema hivi juu ya nguzo, birika la shaba na misingi ya kuliwekea, vinara na vyombo vingine vilivyoachwa katika muji huu,


Wakaldea walivunja vipandevipande nguzo za shaba nyeusi ambazo zilikuwa katika nyumba ya Yawe pamoja na misingi ya birika kubwa la shaba nyeusi lililokuwa katika nyumba ya Yawe, wakapeleka shaba nyeusi yote mpaka Babeli.


Juu ya vitu Solomono alivyotengeneza: nguzo mbili, birika kubwa moja na sanamu za ngombe dume kumi na mbili za shaba nyeusi ambazo zilikuwa chini ya hilo birika kubwa pamoja na misingi, shaba nyeusi ya vitu hivi vyote ilikuwa na uzito mwingi sana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ