Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kisha, akajenga jengo lililoitwa Nyumba ya pori ya Lebanoni. Urefu wake ulikuwa metre makumi ine na ine na nusu, upana wake metre makumi mbili na mbili na sentimetre makumi mbili na tano, na urefu wake wa kwenda juu metre kumi na tatu na nusu. Ilikuwa imejengwa juu ya mistari mitatu ya nguzo za mierezi, nguzo ambazo zilishikilia boriti za mierezi kwa upande wa juu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 7:2
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alitengeneza ngao ndogondogo mia tatu kwa zahabu iliyofuliwa; kilo moja na nusu ilitumiwa kwa kila ngao. Halafu mufalme akaziweka katika jengo lililoitwa Nyumba ya Pori ya Lebanoni.


Vyombo vyote vya kunywa divai vya mufalme Solomono vilikuwa vya zahabu, na vyombo vyote vilivyokuwa katika Nyumba ya Pori ya Lebanoni vilikuwa vya zahabu safi; hakuna kilichotengenezwa kwa feza maana madini ya feza haikuhesabiwa kuwa kitu wakati ule.


Kila mustari ulikuwa na nguzo kumi na tano; basi zote pamoja zilikuwa nguzo makumi ine na tano. Vyumba vilivyojengwa juu ya nguzo hizo, alivitilia dari ya mbao za mierezi.


Mufalme Solomono alipomaliza kujenga nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme na majengo mengine yote aliyokusudia kujenga,


na miji yake yote ya kuwekea akiba, magari yake ya vita, na waaskari wapanda-farasi wake; vilevile na chochote alichotaka kujenga katika Yerusalema, Lebanoni au nafasi ingine katika ufalme wake.


Vilevile alitengeneza ngao ndogondogo mia tatu, kila moja ilipakwa zahabu yapata kilo tatu, halafu mufalme akaziweka katika jengo lililoitwa Nyumba ya Pori la Lebanoni.


Maziba yako ni kama paa mapacha, ni kama swala wawili.


Ulinzi wote wa Yuda uliporomoka. Siku hiyo mulikwenda kutafuta silaha zilizokuwa zimelindwa katika Nyumba ya Pori,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ