Halafu, alifuma nyavu mbili zenye mapambo ya murabamuraba, akatengeneza taji kwa kusokota mukufu: vyote hivyo kwa ajili ya kupamba taji za shaba zilizowekwa juu ya zile nguzo.
Na taji hizo zilizokuwa juu ya nguzo mbele ya baraza, zilipambwa kwa mufano wa maua ya yungiyungi, urefu wa kwenda juu metre moja na sentimetre makumi munane.
Kila nguzo ilikuwa na urefu wa metre nane, na juu yake kulikuwa kichwa cha shaba nyeusi. Urefu wa kila kichwa ulikuwa metre moja na sentimetre makumi mbili na tano. Kila kichwa kilizungushiwa mapambo ya makomamanga, yote ya shaba nyeusi.