Kiwanja cha nyumba ya mufalme kilikuwa na kuta zenye mustari moja wa mbao za mierezi na mistari mitatu ya mawe ya kuchongwa kila moja; ndivyo ilivyokuwa hata kwa kiwanja cha ndani cha nyumba ya Yawe na kwa baraza la nyumba.
Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.