Kuuzunguka ukuta wa inje wa nyumba hiyo, alijenga vyumba kila gorofi ikiwa na urefu wa kwenda juu metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano; navyo vilikuwa vimeunganishwa na nyumba kwa boriti za mierezi.
Na katika mwezi wa Buli, ni kusema mwezi wa nane, katika mwaka wa kumi na mumoja, ujenzi wa nyumba ulimalizika, na kazi ilikuwa imekamilika kama ilivyopangwa. Solomono alitumia miaka saba kwa kujenga.
Mulango wa kuingilia sehemu ya chini ya jengo lililoongezwa kwenye ubavu wa nyumba, ulikuwa upande wa kusini. Ndani, mulikuwa ngazi ambayo watu waliweza kupandia kwa kwenda kwenye gorofi ya katikati na ya mwisho.
Basi, mufalme Solomono akamaliza kazi zote zilizoelekea nyumba ya Yawe. Kisha Solomono akaleta mali yote ambayo baba yake Daudi, alikuwa ameitoa kwa Bwana, ni kusema: feza, zahabu na vyombo; akaiweka katika hazina za nyumba ya Yawe.
Mara tatu kila mwaka, Solomono alitoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya mazabahu aliyokuwa amemujengea Yawe, akamufukizia Yawe ubani. Akafanya vile ilivyofaa kwa nyumba ya Yawe.