Daudi na watu wote wa Israeli, walikuwa wanaimba nyimbo na kucheza kwa nguvu zao zote, mbele ya Yawe. Walipiga ala za muziki zilizotengenezwa na muti wa muvinje: vinubi, vinanda, matari, kayamba na matoazi.
Wale maliwali wake kumi na wawili, kila mumoja kwa mwezi aliopangiwa, walipeleka chakula cha kutosha kwa ajili ya mufalme na wale wote waliokula katika nyumba yake. Mahitaji yao yote yalitoshelezwa.
Upande wa ndani wa kuta za nyumba aliufunika kwa mbao za mierezi, kutokea kwenye sakafu mpaka kwenye boriti za dari; na sakafu akaitandikia mbao za miberoshi.
Mufalme Solomono akawahesabu wageni wote waliokuwa katika inchi ya Israeli. Hesabu hii ni kama ile Daudi baba yake aliyofanya. Kulikuwa wageni yapata elfu mia moja makumi tano na tatu na mia sita.