Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 5:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wale maliwali wake kumi na wawili, kila mumoja kwa mwezi aliopangiwa, walipeleka chakula cha kutosha kwa ajili ya mufalme na wale wote waliokula katika nyumba yake. Mahitaji yao yote yalitoshelezwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 5:7
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Esau alipoinua macho na kuwaona wale wamama na watoto, akauliza: “Ni wa nani hawa unaokuwa nao?” Yakobo akamujibu: “Hawa ni watoto ambao Mungu, kwa neema yake, amenijalia mimi mutumishi wako.”


na kuomba akisema: ‘Asifiwe Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye amemufanya muzao wangu kuwa mufalme kwa pahali pangu, na ambaye amenipa maisha hata nimeyaona mambo hayo.’ ”


Asifiwe Yawe, Mungu wako, ambaye amependezwa nawe, akakuweka juu ya kiti cha kifalme cha Israeli! Kwa sababu Yawe anapenda Israeli milele, amekuweka wewe ukuwe mufalme, kusudi uimarishe haki na sheria ya Mungu.”


Kwa hiyo, ninakuomba unipe mimi mutumishi wako moyo wa hekima nipate kuamua watu wako, niweze kutambua mazuri na mabaya; maana ni nani anayeweza kuhukumu watu wako wanaokuwa wengi hivi?”


Solomono alichagua maliwali kumi na wawili kwa inchi nzima ya Israeli. Hao walipewa kazi ya kutafuta chakula kwa ajili ya mufalme na nyumba yake. Kila mumoja wao alileta chakula kutoka jimbo lake kwa mwezi mumoja kila mwaka.


Solomono alikuwa na vibanda elfu makumi ine kwa ajili ya farasi wa magari yake ya kukokotwa, na waaskari wapanda-farasi elfu kumi na mbili.


Zamu ya kila mumoja ilipofika, alipeleka vilevile shayiri na majani ya kulisha farasi na nyama wanaokimbia mbio.


Ulimi wangu ukuwe muzito, kama nisipokukumbuka wewe, ee Yerusalema, nisipokufurahia kuliko furaha yangu kubwa!


Hizi ni mezali za Solomono: Mutoto mwenye hekima ni furaha ya baba yake; lakini mutoto mupumbafu ni huzuni ya mama yake.


Mutoto mwenye hekima anasikia maagizo ya baba yake, lakini mwenye kiburi hasikilizi maonyo.


Mutoto mwenye hekima anamufurahisha baba yake, lakini mupumbafu anamuzarau mama yake.


Baba wa mutoto mwenye haki atajaa furaha; anayezaa mutoto mwenye hekima atamufurahia.


Mimi pamoja na watoto Yawe alionipa ni kitambulisho na mufano katika Israeli kwa jina la Yawe wa majeshi anayekaa kwenye mulima Sayuni.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ