Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 5:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Solomono alikuwa na vibanda elfu makumi ine kwa ajili ya farasi wa magari yake ya kukokotwa, na waaskari wapanda-farasi elfu kumi na mbili.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 5:6
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kanana alikuwa babu ya Sidona, muzaliwa wake wa kwanza, na Heti,


Solomono alikusanya magari ya vita na waaskari wapanda-farasi. Alikuwa na magari ya vita elfu moja na mia ine na waaskari wapanda-farasi elfu kumi na mbili ambao aliwaweka katika miji yenye vituo vya magari ya vita, na kule Yerusalema.


Wale maliwali wake kumi na wawili, kila mumoja kwa mwezi aliopangiwa, walipeleka chakula cha kutosha kwa ajili ya mufalme na wale wote waliokula katika nyumba yake. Mahitaji yao yote yalitoshelezwa.


Chumba cha ndani, kilichoitwa Pahali Patakatifu Sana, kilijengwa katika sehemu ya nyuma ya nyumba. Kilikuwa kimejengwa kwa mbao za mierezi kutokea kwenye sakafu mpaka kwenye dari, na urefu wake ulikuwa metre tisa.


Chumba hicho kilikuwa na metre tisa urefu, metre tisa upana, na metre tisa kwenda juu; nacho kilipambwa kwa zahabu safi. Vilevile, alitengeneza mazabahu kwa mbao za mierezi.


na miji yake yote ya kuwekea akiba, magari yake ya vita, na waaskari wapanda-farasi wake; vilevile na chochote alichotaka kujenga katika Yerusalema, Lebanoni au nafasi ingine katika ufalme wake.


Naye mufalme Hiramu akawatuma wafundi wake wenye kujua bahari pamoja na watumishi wa Solomono.


Mbao za mierezi ambazo Daudi aliletewa na Wasidoni na Watiro zilikuwa hazihesabiki.


Solomono alikusanya magari ya vita na waaskari wapanda-farasi; alikuwa na magari ya vita elfu moja na mia ine, na waaskari wapanda-farasi elfu kumi na mbili. Aliwaweka katika miji yenye vituo vya magari ya vita na kwake katika Yerusalema.


Naye Hiramu, mufalme wa Tiro, akamujibu Solomono kwa barua akisema: “Kwa sababu Yawe anawapenda watu wake, amekufanya kuwa mufalme wao.


kusudi wanipasulie mbao kwa wingi, maana nyumba ninayokusudia kujenga ni kubwa na ya ajabu.


Watu walitoa feza za kuwalipa waseremala na wajengaji, walitoa vilevile chakula, vinywaji na mafuta, kusudi vipelekwe katika miji ya Tiro na Sidona kubadilishwa na miti ya mierezi kutoka Lebanoni. Miti hiyo ililetwa kwa njia ya bahari mpaka Yopa. Haya yote yalifanyika kwa musaada wa mufalme Kiro wa Persia.


Sauti ya Yawe inavunja miti mikubwa ya mierezi; Yawe anavunja mierezi ya Lebanoni.


Kisha nikawaambia: Kama mukipendezwa, munilipe mushahara wangu; lakini kama munaona sivyo, basi muache. Basi, wakanipimia vikoroti makumi tatu vya feza kwa mushahara wangu.


Musimurudishie mutu ubaya kwa ubaya. Mukuwe na roho ya kufanya mema mbele ya watu wote.


Lakini kila mutu kati yetu alipokea neema kadiri ya kipimo alichojaliwa na Kristo.


Hata hivyo, asikuwe na farasi wengi kwa ajili yake mwenyewe, wala asiwarudishe watu Misri kwa kujipatia farasi zaidi, kwa sababu Yawe amewaonya: ‘Hamutarudi tena kwa njia ile.’


Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ