Lakini neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: ‘Wewe umemwanga damu nyingi na kupigana vita kubwa. Kwa sababu ya damu nyingi ambayo umemwanga mbele yangu hapa katika dunia, hautanijengea nyumba.
Halafu mufalme Daudi akasimama na kusema: “Enyi wandugu zangu na watu wangu, munisikilize. Nilikusudia ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Sanduku la Agano la Yawe, kiti cha kuwekea miguu ya Mungu wetu; na nilifanya matayarisho ya kujenga.
chakula kilichotayarishwa kwenye meza yake, jinsi wakubwa wake walivyokaa kwenye meza, kazi ya watumishi wake na namna walivyovaa, wenye kuleta vinywaji na jinsi walivyovaa, na sadaka za kuteketeza ambazo alitoa katika nyumba ya Yawe.
Zaidi ya hayo, kila siku niliwakulisha watu mia moja na makumi tano, kati yao kukiwa Wayuda na wakubwa zaidi ya wale watu waliotufikia toka mataifa jirani.
Kila siku, kwa kuwalisha watu hao, nilichinjiwa ngombe dume mumoja na kondoo safi sita na kuku. Kila mara kisha siku kumi nilitoa divai kwa wingi. Lakini zaidi ya haya yote, kwa sababu watu walikuwa na muzigo muzito wa kubeba kila siku, sikutaka posho ya zaidi.
Wafalme hao walipoletwa, Yoshua akawaita Waisraeli wote na wakubwa wa waaskari waliokwenda naye kwa vita, akawaambia: “Mukuje karibu muwakanyage wafalme hawa kwenye shingo yao.” Nao wakasogea na kuwakanyaga kwenye shingo.