Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 4:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Solomono alichagua maliwali kumi na wawili kwa inchi nzima ya Israeli. Hao walipewa kazi ya kutafuta chakula kwa ajili ya mufalme na nyumba yake. Kila mumoja wao alileta chakula kutoka jimbo lake kwa mwezi mumoja kila mwaka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 4:7
6 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Baba yako alitubebesha muzigo muzito. Basi, utupunguzie muzigo huo muzito wa baba yako, nasi tutakutumikia.”


Haya ndiyo majina ya hao maliwali: Beni-Huri alisimamia sehemu ya milima ya Efuraimu. Beni-Dekari alisimamia miji ya Makasi, Salabimu, Beti-Semesi na Eloni-Beti-Hanani. Beni-Hesedi alisimamia muji wa Aruboti, alisimamia vilevile Soko na inchi yote ya Heferi. Beni-Abinadabu, mume wa Tafati, binti ya Solomono, alisimamia jimbo lote la Dori. Bana mwana wa Ahiludi, alisimamia miji ya Tanaki, Megido, na sehemu yote ya Beti-Seani inayokuwa karibu na muji wa Zaretana, upande wa kusini wa muji wa Yezereheli, na kutoka Beti-Seani mpaka miji ya Abeli-Mehola, na hata kupita muji wa Yokimamu. Beni-Geberi alisimamia muji wa Ramoti-Gileadi pamoja na vijiji vya Gileadi vilivyokuwa vya Yairi mwana wa Manase; tena alisimamia jimbo la Argobu katika inchi ya Basani; yote kwa jumla ilikuwa miji mikubwa makumi sita iliyozungushiwa kuta na kuwekwa vifungio vya shaba kwenye mulango. Ahinadabu mwana wa Ido, alisimamia jimbo la Mahanaimu. Ahimasi, mume wa Basemati, binti ya Solomono, alisimamia sehemu ya inchi ya Nafutali. Bana mwana wa Husayi, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Aseri na Bealoti. Yosafati mwana wa Parua, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Isakari. Simei mwana wa Ela, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Benjamina. Geberi mwana wa Uri, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Gileadi, ambayo zamani ilitwaliwa na Sihoni mufalme wa Waamori, na Ogu mufalme wa Basani. Zaidi ya hawa kumi na wawili, kulikuwa mukubwa mumoja aliyesimamia inchi nzima ya Yuda.


Wale maliwali wake kumi na wawili, kila mumoja kwa mwezi aliopangiwa, walipeleka chakula cha kutosha kwa ajili ya mufalme na wale wote waliokula katika nyumba yake. Mahitaji yao yote yalitoshelezwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ