Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1-6 Solomono alikuwa mufalme wa inchi yote ya Israeli, na hawa ndio walikuwa wakubwa wa serikali yake wenye vyeo vya juu: Azariya mwana wa Zadoki alikuwa kuhani. Elihorefu na Ahiya, wana wa Sisa, walikuwa wakatibu. Yosafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwandishi wa habari. Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa jemadari wa waaskari. Zadoki na Abiatari walikuwa makuhani. Azariya mwana wa Natani alikuwa mukubwa wa maliwali. Kuhani Zabudi mwana wa Natani alikuwa rafiki ya mufalme. Ahisari alikuwa mukubwa wa nyumba ya mufalme. Adoniramu mwana wa Abuda alikuwa musimamizi wa kazi za kulazimishwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 4:1
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa Yoabu alikuwa jemadari wa waaskari wote wa Waisraeli. Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa jemadari wa Wakereti na Wapeleti.


Kule Hebroni, alitawala watu wa Yuda kwa muda wa miaka saba na miezi sita, na kule Yerusalema alitawala watu wa Israeli pamoja na Yuda kwa muda wa miaka makumi tatu na mitatu.


Kwa hiyo, Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akawahukumu watu wake wote kufuatana na haki na sheria.


Hata yeye sitamunyanganya urizi wote, lakini nitamwachia mwana wako kabila moja, kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi, na kwa ajili ya Yerusalema ambao nimeuchagua kuwa wangu.”


Nyuma Rehoboamu alitaka kujua maoni ya wazee ambao walikuwa washauri wa baba yake Solomono alipokuwa angali muzima, akawauliza: “Munanishauria niwape jibu gani watu hawa?”


Watu wote wa Israeli waliposikia juu ya hukumu ya mufalme, walimwogopa. Wakatambua kwamba alikuwa na hekima ya Mungu iliyomuwezesha kutoa hukumu za haki.


Kutoka kabila la Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase kutoka ngambo ya muto Yordani: watu elfu mia moja na makumi mbili wenye kila aina ya silaha za vita.


Basi, Solomono akaondoka pahali pale pa kuabudia, kule Gibeoni, kulipokuwa hema la mukutano, akarudi Yerusalema. Akatawala inchi ya Israeli.


Solomono alitawala inchi yote ya Israeli kwa miaka makumi ine.


Si Solomono alitenda zambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Yeye alikuwa mufalme mukubwa kuliko wafalme wa mataifa mengine. Mungu akamupenda na akamufanya kuwa mufalme juu ya watu wote wa Israeli, hata hivyo wanawake wa mataifa mengine, wakamusukuma kutenda zambi.


Mimi Muhubiri, nilikuwa mufalme wa Israeli, kule Yerusalema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ