Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 3:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Solomono akamwambia: “Ulimwonyesha wema mwingi mutumishi wako Daudi, baba yangu, kwa sababu alikutumikia kwa uaminifu, kwa haki na kwa moyo wa usawa; na umedumisha mema yako kwa kumupa mwana anayeikaa sasa kwenye kiti chake cha kifalme.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 3:6
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini yeye akasema: ‘Yawe aliyeniongoza katika maisha yangu, atamutuma malaika wake aende pamoja nawe na kukufanikisha katika safari yako. Nawe utamutwalia mwana wangu muke kutoka kwa jamaa yangu na nyumba ya baba yangu.


Yawe alinitendea kwa kadiri ya haki yangu; alinilipa kwa vile mikono yangu haina kosa.


Yawe amenilipa kwa kadiri ya haki yangu, kwa kadiri ya usafi wangu mbele yake.


“Kwenda umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe anasema hivi: Si wewe utakayenijengea nyumba ya kukaa.


na kuomba akisema: ‘Asifiwe Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye amemufanya muzao wangu kuwa mufalme kwa pahali pangu, na ambaye amenipa maisha hata nimeyaona mambo hayo.’ ”


Yawe alifanya hivyo kwa sababu Daudi alitenda mema mbele yake na hakuenda pembeni ya maagizo ya Yawe siku za maisha yake yote, isipokuwa tu lile jambo la Uria Muhiti.


Naye Yawe atatimiza ahadi yake aliyotoa aliponiambia kwamba, ikiwa wazao wangu watatii amri zake na kumutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wote, hakutakosekana mumoja wao kwa kutawala Israeli nyakati zote.


Tena kama ukifuata njia yangu na kushika masharti na amri zangu kama vile baba yako Daudi alivyofanya, basi, nitakupa maisha marefu.”


Nawe kama ukinitumikia kwa ukamilifu wa moyo na usawa kama baba yako Daudi alivyofanya, ukitii amri zangu na kutimiza yale yote niliyokuamuru, ukifuata masharti yangu na maagizo yangu,


“Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote na kutenda mazuri mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.


Solomono akamwambia Mungu: “Ulimutendea baba yangu Daudi mema mengi, na umenijalia kuwa mufalme kwa pahali pake.


Ukuwe na utulivu mukubwa, ee nafsi yangu, kwa vyote Yawe amenitendea.


Unitendee mimi mutumishi wako kwa wema, nipate kuishi na kushika neno lako.


Lakini mimi ninatumainia wema wako, moyo wangu ufurahie wokovu wako. Nitakuimbia wewe, ee Yawe, kwa vyote ulivyonitendea!


Ni mutu anayefanya hivi: anaishi katika ukamilifu, anatenda kwa haki siku zote, anasema ukweli kutoka ndani ya moyo, hatetani, hatendei rafiki yake uovu, hamutukani jirani yake, anazarau wapotevu, anaheshimu wanaomwabudu Yawe, hageuzi kiapo chake hata kikimuletea hasara, hakopeshi feza yake kwa kupata faida, wala kupokea kituliro kumutesa asiyekuwa na kosa. Mutu anayefanya vile, hatatikisika hata kidogo.


Lakini juu ya mutumishi wangu Musa, hali ni tofauti kabisa. Yeye ana madaraka ya kuwatunza watu wangu wote.


Hivi mutakuwa watajiri katika vitu vyote, kusudi siku zote muweze kuonyesha moyo wa kutoa, hata watu wengi watamushukuru Mungu kwa ajili ya musaada tunaowafikishia kutoka kwenu.


Ni hivi niliona kuwa ni vizuri kuwashauri wandugu hawa watangulie kufika kwenu mbele yangu kusudi watayarishe vile vitu mulivyoahidi kutoa kwa mapenzi yenu. Hivi vitakuwa tayari na itaonyesha kwamba mumevitoa kwa moyo mwema, wala si kwa uchoyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ