Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Wakati mumoja, Solomono alikwenda kutoa sadaka kule kwenye kilima cha Gibeoni, maana palikuwa ndipo pahali pakubwa pa ibada. Ilikuwa ni kawaida ya Solomono kutoa maelfu ya sadaka za kuteketezwa katika mazabahu hiyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 3:4
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walawi na makuhani walihamisha Sanduku la Agano na hema la mukutano, na vyombo vitakatifu vyote vilivyokuwa mule ndani ya hema.


Naye Solomono alimutolea Yawe sadaka za amani: ngombe elfu makumi mbili na mbili na kondoo elfu mia moja na makumi mbili. Hivi ndivyo mufalme na watu wote wa Israeli walivyozindua nyumba ya Yawe.


Yawe alimutokea tena kama alivyomutokea kule Gibeoni.


Mufalme Daudi akawaweka kuhani Zadoki na makuhani wenzake kuwa watumishi wa hema ya Yawe iliyokuwa pahali pa kuabudia kule Gibeoni


Hema la Yawe ambalo lilitengenezwa na Musa katika jangwa, na mazabahu ya sadaka ya kuteketezwa, wakati ule vilikuwa bado pale pahali pa kuabudia kule Gibeoni.


Mufalme Solomono aliita majemadari wote wa vikundi vya maelfu na vya mamia, waamuzi, viongozi wote wa ukoo za Waisraeli.


Kisha akaandamana nao mpaka pahali pa ibada kule Gibeoni. Walikwenda kule kwa sababu pale ndipo pahali palipokuwa hema la mukutano la Mungu ambalo Musa mutumishi wa Yawe, alilotengeneza katika jangwa.


Mufalme Hezekia wa Yuda akawapa watu waliokusanyika jumla ya ngombe dume elfu moja na kondoo elfu saba. Vilevile, wakubwa wakawapa ngombe dume elfu moja na kondoo elfu kumi. Hesabu kubwa ya makuhani wakajitakasa.


Naye Solomono akamutolea ngombe elfu makumi mbili na mbili na kondoo elfu mia moja makumi mbili. Hivi ndivyo Solomono na watu wote walivyozinduwa nyumba ya Mungu.


Kuni zote za Lebanoni na nyama wake wote havitoshi kwa sadaka ya kuteketezwa mbele yake.


Katika mwaka uleule, maana yake mwaka wa ine wa utawala wa mufalme Zedekia juu ya Yuda, katika mwezi wa tano, Hanania, mwana wa Azuri, nabii kutoka muji Gibeoni, alisema nami katika nyumba ya Yawe. Alisema nami mbele ya makuhani na watu wote, akiniambia kwamba


Habari hizo zilisababisha hofu kubwa kule Yerusalema kwa sababu muji wa Gibeoni ulikuwa mukubwa sana kati ya miji ya kifalme. Muji huu ulikuwa vilevile mukubwa kuliko Ai na wanaume wake wote walikuwa waaskari hodari sana.


Miji ya ukoo za kabila la Benjamina ni: Yeriko, Beti-Hogla, Emeki-Kesisi, Beti-Araba, Zemaraimu, Beteli, Awimu, Para, Ofura, Kefari-Amoni, Ofuni na Geba. Jumla ya miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake. Gibeoni, Rama, Beroti, Misipa, Kefira, Moza, Rekemu, Iripeli, Tarala, Zela, Ha-Elefu, Yebusi, ni kusema Yerusalema, Gibea na Kiriati-Yearimu. Jumla ya miji kumi na mine pamoja na vijiji vyake. Hiyo yote ni sehemu watu wa kabila la Benjamina na ukoo zao waliyopewa.


Lakini wakaaji wa Gibeoni walipopata habari juu ya jinsi Yoshua alivyoitendea miji ya Yeriko na Ai,


Basi, Saulo akawaambia watu: “Muniletee sadaka yenu ya kuteketezwa na zile za amani.” Naye akatolea sadaka ya kuteketezwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ