Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Solomono alimupenda Yawe, akashika masharti ya baba yake Daudi; lakini tu, naye alitoa sadaka na kufukiza ubani juu ya vilima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 3:3
51 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, sitamunyanganya urizi wote, wala sitamwondolea mamlaka wakati angali anaishi, kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi ambaye nilimuchagua, na ambaye alifuata amri zangu na masharti yangu.


Na kama utashika yote nitakayokuamuru, kama utaishi kulingana na mapenzi yangu, kama utatenda mema mbele yangu kwa kushika masharti yangu na amri zangu, kama vile mutumishi wangu Daudi alivyofanya, mimi nitakuwa pamoja nawe siku zote. Na nitakupatia inchi ya Israeli na kuufanya utawala wako ukuwe imara kama nilivyomufanyia Daudi.


Maana, alipokuwa muzee, wake zake walimupotosha hata akaitumikia miungu mingine, wala hakukuwa mwaminifu kabisa kwa Yawe, Mungu wake, kama baba yake Daudi alivyokuwa mwaminifu.


Hivyo, Solomono alitenda maovu mbele ya Yawe, wala hakufuata kwa ukamilifu mapenzi ya Yawe kama baba yake Daudi alivyokuwa amefanya.


Walijitengenezea vilevile pahali pa ibada, minara ya kutambikia, na sanamu za Ashera, juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wenye majani mengi.


nikaunyanganya ufalme utoke kwa wazao wa Daudi, nikakupa wewe. Lakini wewe ni kinyume kabisa cha mutumishi wangu Daudi ambaye alizishika amri zangu. Alifuata mapenzi yangu kwa moyo wake wote na kutenda tu yanayokuwa sawa mbele ya macho yangu.


Mufalme Asa alitenda mambo yanayokuwa mema mbele ya Yawe kama vile Daudi babu yake alivyofanya.


Lakini nafasi ya kutambikia miungu juu ya vilima haikuharibiwa. Hata hivyo, yeye alikuwa na moyo mwaminifu kwa Yawe maisha yake yote.


Abiyamu alitenda zambi zilezile baba yake alizotenda, wala hakukuwa na moyo mwaminifu kwa Yawe, Mungu wake, kama babu yake Daudi alivyokuwa.


Yawe alifanya hivyo kwa sababu Daudi alitenda mema mbele yake na hakuenda pembeni ya maagizo ya Yawe siku za maisha yake yote, isipokuwa tu lile jambo la Uria Muhiti.


Alitenda mema mbele ya Yawe kama vile baba yake Asa alivyofanya.


Lakini hakuharibu nafasi ya kutambikia juu ya vilima. Watu waliendelea kutambikia na kufukiza ubani kwa nafasi ile.


Tena kama ukifuata njia yangu na kushika masharti na amri zangu kama vile baba yako Daudi alivyofanya, basi, nitakupa maisha marefu.”


Solomono akamwambia: “Ulimwonyesha wema mwingi mutumishi wako Daudi, baba yangu, kwa sababu alikutumikia kwa uaminifu, kwa haki na kwa moyo wa usawa; na umedumisha mema yako kwa kumupa mwana anayeikaa sasa kwenye kiti chake cha kifalme.


Kwa hiyo, sasa, ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba vilevile utimize ile ahadi uliyomwahidi mutumishi wako Daudi, baba yangu, ukisema: ‘Siku zote utakuwa na mutu mumoja wa uzao wako kwa kuikaa katika kiti cha kifalme cha Israeli, ikiwa wazao wako watakuwa waangalifu juu ya mwenendo wao mbele yangu kama wewe ulivyofanya mbele yangu.’


Nanyi, mukuwe waaminifu kwa Yawe, Mungu wetu, mukifuata masharti yake na kutii amri zake zote kama munavyofanya hivi leo.”


Nawe kama ukinitumikia kwa ukamilifu wa moyo na usawa kama baba yako Daudi alivyofanya, ukitii amri zangu na kutimiza yale yote niliyokuamuru, ukifuata masharti yangu na maagizo yangu,


Wakati wa maisha yake yote alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kwa sababu kuhani Yehoyada alikuwa akimufundisha.


Hata hivyo, nafasi za kuabudu miungu kwenye milima hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani kule.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, lakini hakukuwa kama babu yake Daudi. Akafanya mambo yote kama vile baba yake Yoasi.


Nafasi za kutambikia kwenye milima hazikuharibiwa na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani kwa nafasi zile.


Hata hivyo, nafasi za kutambikia miungu ya uongo hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambikia na kufukiza ubani kwenye nafasi za juu. Yotamu alijenga mulango wa kaskazini wa nyumba ya Yawe.


Hata hivyo, nafasi za kutambikia kwenye milima hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani pale.


Lakini hata kama mukiniambia: ‘Tunamutegemea Yawe, Mungu wetu’, si huyohuyo ambaye Hezekia aliziharibu nafasi zake zote za kuabudu kwenye vilima pamoja na mazabahu zake na kuwaambia watu wa Yuda na Yerusalema: Munapaswa kuabudu mbele ya mazabahu hii ya Yerusalema tu?


Aliharibu nafasi zote za kuabudu miungu na kuvunja nguzo na kukata Ashera. Vilevile, alivunja nyoka ya shaba ambayo Musa alitengeneza, iliyoitwa Nehustani. Mpaka wakati ule, watu wa Israeli walikuwa wakiitambikia.


Lakini hata hivyo pahali pa kutambikia miungu mingine katika Israeli hapakuharibiwa; lakini yeye alikuwa na moyo mwaminifu maisha yake yote.


Yawe anawalinda wote wanaomupenda; lakini anawaangamiza waovu wote.


Nami niliogopa na kuzani kwamba ulikuwa umenitupa; kumbe, ulisikia kilio changu nilipokuita unisaidie.


Agizo hili linalazimisha Waisraeli kuletea Yawe nyama ambao wanawachinja katika mashamba. Wataleta nyama wale kwa kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano, naye atawachinja na kumutolea Yawe sadaka za amani.


Yesu akamujibu: “ ‘Umupende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote na kwa akili yako yote.’


“Kama munanipenda, mutashika amri zangu.


“Anayekubali amri zangu na kuzitii, ni yeye anayenipenda. Baba yangu atamupenda yule anayenipenda, na mimi nitamupenda vilevile na nitajitambulisha kwake.”


Tunajua kwamba katika mambo yote Mungu anatumika kwa kuwajalia wale wanaomupenda, ndio wale walioitwa naye kufuatana na kusudi lake.


Lakini yule anayemupenda Mungu, huyu anajulikana naye.


“Sasa, enyi Waisraeli, Yawe, Mungu wenu, anataka nini kwenu? Yawe, Mungu wenu, anataka mumwogope, mufuate njia zake zote, mumupende, mumutumikie Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wote na kwa roho yenu yote,


na mutii amri na masharti ya Yawe ninayowawekea leo, kwa mafaa yenu wenyewe.


“Basi, mukitii amri zangu ninazowapa leo, mukimupenda Yawe, Mungu wenu, na kumutumikia kwa moyo wenu wote na kwa roho yenu yote,


Kama mukitii amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa leo, mukimupenda Yawe, Mungu wenu, na kufuata njia zake na kushika amri, masharti na maagizo yake, basi, mutaishi na kuongezeka; naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika inchi ambayo munakwenda kuirizi.


Mumupende Yawe, Mungu wenu. Muitii sauti yake na kuambatana naye. Kama munafanya hivyo, mutapata maisha marefu na kuishi katika inchi ambayo Yawe aliwaahidi wazee wenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo, kwamba atawapa.”


Yawe, Mungu wenu, atawafanya ninyi na wazao wenu mukuwe na moyo wa utii kusudi mumupende yeye kwa moyo wenu wote na roho yenu, mupate kuishi.


Mumupende Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote, kwa roho yenu yote na kwa nguvu yenu yote.


Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


Wale wabinti wakawajibu: “Ndiyo, yuko. Tena yuko mbele yenu; mukifanya haraka mutamukuta. Ameingia katika muji leo tu, kwa sababu leo watu watatoa sadaka kule kwenye mulima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ