Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Solomono alifanya mapatano na mufalme wa Misri, kwa kumwoa binti yake. Akamuleta binti wa mufalme wa Misri na kumuweka katika muji wa Daudi, mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake mwenyewe, nyumba ya Yawe, na ukuta wa kuuzunguka Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 3:1
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, mufalme Daudi aliteka kikingio cha Sayuni, ni kusema muji wa Daudi.


Solomono alipenda sana wanawake wa kigeni: binti ya mufalme wa Misri, wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni, na Wahiti,


Solomono alianza kujenga nyumba ya Yawe katika mwaka wa mia ine na makumi nane kisha Waisraeli kutoka Misri. Huo ulikuwa mwaka wa ine wa utawala wa Solomono juu ya Israeli, katika mwezi wa Zivu, ni kusema mwezi wa pili.


Solomono alijijengea nyumba ya kifalme, naye alitumia muda wa miaka kumi na mitatu kwa kuimaliza.


Nyumba yake ya kukaa mwenyewe iliyokuwa nyuma ya Uwanja wa Hukumu. Ilijengwa kama zile zingine. Solomono alijenga vilevile nyumba kama uwanja huo kwa ajili ya binti ya mufalme wa Misri, ambaye alikuwa amemwoa.


Mufalme Solomono alipomaliza kujenga nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme na majengo mengine yote aliyokusudia kujenga,


Kisha miaka makumi mbili ambayo Solomono alipitisha kwa kuzijenga nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme,


Kisha binti ya mufalme wa Misri alihama katika muji wa Daudi, akaenda kukaa katika nyumba yake mwenyewe ambayo Solomono alimujengea. Kisha Solomono akajenga uwanja wa Milo.


Daudi alikaa katika makimbilio yale, na kwa hiyo, muji ule ukaitwa “Muji wa Daudi.”


Wakati mufalme Yosafati wa Yuda alipokuwa amekwisha kuwa mutu tajiri na mwenye heshima, alifanya mupango wa ndoa kati ya jamaa yake, na jamaa ya mufalme Ahabu wa Israeli.


Solomono alimuhamisha binti wa mufalme wa Misri, kutoka muji wa Daudi, akamupeleka kwenye nyumba aliyomujengea. Akasema: “Muke wangu hataishi katika nyumba ya Daudi mufalme wa Israeli, kwa maana pahali pote ambapo sanduku la Yawe limekuwa, ni patakatifu.”


Wao wakatujibu hivi: “Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na dunia, na tunaijenga upya nyumba ambayo ilikuwa imejengwa na kumalizika pale mbele na mufalme mumoja mukubwa wa Israeli.”


Tutavunja amri zako tena na kuoana na watu hawa wanaotenda maovu haya? Hautatukasirikia na kutuangamiza kabisa, na kusibaki hata mumoja wetu muzima wala yeyote wa kutoroka?


“Musiwachukie Waedomu; hao ni wandugu zenu. Na musiwachukie Wamisri, maana mulikaa katika inchi yao kama vile wageni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ