Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Timiza maagizo ya Yawe, Mungu wako, ufuate njia zake na kushika masharti yake, amri zake, maagizo yake na maamuzi yake kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa. Kwa hiyo, utafanikiwa katika kila jambo unalofanya na kokote unakoenda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 2:3
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akaweka kambi za waaskari katika inchi ya Edomu yote. Nao Waedomu wote wa kule wakakuwa watumishi wake. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Halafu Daudi aliweka kambi za waaskari katika muji wa Waaramu wa Damasiki. Basi, Waaramu wakakuwa watumishi wake na wakakuwa wanamulipa kodi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Solomono alimupenda Yawe, akashika masharti ya baba yake Daudi; lakini tu, naye alitoa sadaka na kufukiza ubani juu ya vilima.


Basi, Yawe alikuwa pamoja naye, na alimwezesha kwa kila jambo alilotenda. Alimwasi mufalme wa Asuria na kukataa kumutumikia.


Umujalie Solomono mwana wangu kusudi kwa moyo wote ashike amri zako, ushuhuda na maagizo yako, atimize yote na apate kujenga nyumba hii ya utukufu niliyoifanyia matayarisho.”


Maagizo yako ni urizi mukubwa kwangu milele; hayo ni furaha ya moyo wangu.


Heri wanaoshika maagizo yake, wanaomutafuta kwa moyo wao wote,


Linatokea kwa upande mumoja, na kuzunguka mpaka upande mwingine; hakuna kinachoweza kuepuka joto lake.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Mutabaki kwenye mulango wa hema la mukutano usiku na muchana kwa muda wa siku saba, mukifanya mambo Yawe aliyoamuru, kama sivyo mutakufa. Ndivyo nilivyoamuriwa na Yawe.


Kwa hiyo mukuwe waangalifu kushika maneno yote ya agano hili kusudi mupate kufanikiwa katika kazi zenu zote.


“Leo, mumesimama mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi wote viongozi wa makabila, wazee wenu, wakubwa wenu,


Musa akaendelea kusema: “Mushike basi na kufuata masharti na maagizo niliyowafundisha, kusudi mupate kuishi na kurizi inchi ambayo Yawe, Mungu wa babu zenu, anawapa.


Haya ndiyo maagizo, masharti na maamuzi ambayo Musa aliwaambia Waisraeli walipotoka Misri,


“Muangalie! Nimewafundisha masharti na maagizo kama vile Yawe, Mungu wangu alivyoniamuru nifanye, kusudi muyashike katika inchi munayokwenda kuirizi.


Wala hakuna taifa lingine lolote hata likuwe kubwa namna gani, lenye masharti na maagizo ya haki, kama hayo ambayo nimewafundisha siku hii ya leo.


Musa akawaita pamoja Waisraeli, akawaambia: “Enyi Waisraeli, musikilize masharti na maagizo ambayo ninayasema mbele yenu leo. Mujifunze hayo na kuyatimiza kwa uangalifu.


Mukuwe waangalifu kutii amri na sheria ambazo Musa, mutumishi wa Yawe, aliwaamuru: mumupende Yawe, Mungu wenu, mufuate anachotaka na kushika amri zake, mukae pamoja naye na kumutumikia kwa moyo wote na roho yote.”


Kwa hiyo, mukuwe imara katika kushika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa, musiyaache hata kidogo.


Daudi alifanikiwa katika kila kitu alichofanya, maana Yawe alikuwa pamoja naye.


Waaskari wa Wafilistini walikwenda kupigana na Waisraeli, lakini kila mara walipopigana vita, Daudi alipata ushindi kuliko watumishi wa Saulo. Hivyo jina la Daudi likazidi kusifiwa sana.


Kokote Daudi alikotumwa na Saulo, Daudi alifanikiwa. Hivyo, Saulo akamufanya kuwa mukubwa wa waaskari wake. Jambo hilo liliwafurahisha watu wote hata watumishi wa Saulo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ