Wakati wa kufa kwake ulipokaribia, Yakobo akamwita mwana wake Yosefu, akamwambia: “Sasa, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, weka mukono wako chini ya mapaja yangu, uniahidi kwamba utanitendea kwa wema na uaminifu. Usinizike huku Misri,
“Siku zako zitakapotimia na utakapokufa na kujiunga na babu zako, nitamufanya mumoja wa watoto wako wewe mwenyewe akuwe mufalme, nami nitauimarisha ufalme wake.
Basi, mufalme Solomono akaagiza Adonia aitwe kutoka katika hema, akuje kwake. Adonia akafika mbele ya mufalme, akainama kwa heshima. Mufalme akamwambia: “Kwenda kwa nyumba yako.”
Yawe akamwambia Musa: “Siku yako ya kuaga dunia imekaribia. Umwite Yoshua, mukuje pamoja katika hema la mukutano kusudi nimupe maagizo.” Basi, Musa na Yoshua wakaenda katika hema la mukutano,
Kisha Yawe akamwagiza Yoshua, mwana wa Nuni, akamwambia: “Ukuwe imara na hodari, maana utawaongoza Waisraeli katika inchi ambayo nimewaapia kuwapa, nami nitakuwa pamoja nawe.”
Timoteo mwana wangu, ninakupa agizo hili kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Maneno hayo ndiyo yatakayokuwezesha kupiga vita nzuri,