Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 17:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Vibombobombo wakakuwa wanamuletea mukate na nyama, asubui na magaribi; akapata na maji ya kunywa katika kijito kile.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 17:6
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Muzee akaenda, akaikuta maiti ya mutu wa Mungu katika barabara, simba na punda wake pembeni yake. Yule simba hakuikula maiti wala hakumushambulia punda.


Basi, Elia akatii agizo la Yawe, akaenda kukaa kwenye kijito cha Keriti kinachokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani.


Lakini, nyuma ya siku chache kijito kikakauka kwa sababu hakukunyesha mvua katika inchi.


Elia alipoangalia, akaona mukate uliokaangwa juu ya makaa, na chupa ya maji karibu na kichwa chake. Basi, akakula, akakunywa na akalala tena.


Elia akaamuka, akakula na kunywa. Kisha akatembea kwa nguvu ya chakula hicho mwendo wa siku makumi ine, muchana na usiku, mpaka Horebu kwenye mulima wa Mungu.


Yawe anawaangalia wale wanaomwabudu, watu ambao wanatumainia wema wake.


Hawatafezeheka nyakati mbaya zikiwafikia; siku za njaa watakuwa na chakula tele.


Umutumainie Yawe na kutenda mazuri, upate kuishi katika inchi na kuwa salama.


Waisraeli walikula mana kwa muda wa miaka makumi ine, mpaka walipofika katika inchi iliyofaa kwa kuishi, ni kusema mpaka walipovuka mupaka wa Kanana.


Mutu wa namna hiyo anaishi kwenye nafasi ya juu, pahali salama, penye pango na mawe makubwa; atapewa chakula chake siku zote, na maji yake ya kunywa hayatakosekana.


Basi, mufalme Zedekia akatoa amri Yeremia awekwe katika chumba cha walinzi na kupewa mukate kila siku kutoka kwa wapikaji wa mukate mpaka mikate ilipotoweka kabisa huko katika muji. Basi, Yeremia alibaki katika chumba cha walinzi.


Basi! Leo ninafungua minyororo toka mikono yako. Kama unaona ni vizuri kwenda pamoja nami mpaka Babeli, basi tuende pamoja; mimi nitakutunza vizuri. Lakini kama unaona si vizuri kwako kwenda pamoja nami mpaka Babeli, basi, usikuje. Ujue kwamba unaweza kwenda popote katika inchi hii. Basi kwenda kwenye unaona ni vizuri kwenda.


Yawe akamujibu Musa: Uwezo wangu umepunguka? Utaona basi kama neno langu litakuwa la kweli kwako au hapana.


Yesu akawaangalia na kuwaambia: “Jambo hilo haliwezi kutendeka kwa uwezo wa mwanadamu, lakini kwa uwezo wa Mungu, yote yanawezekana.”


Halafu Yesu akawauliza wanafunzi wake: “Nilipowatuma pasipo kubeba feza, wala mufuko, wala viatu, mulikosewa na kitu gani?” Wakamujibu: “Hakuna.”


Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.


Nao wakamwambia: “Sasa tega tusikie.” Samusoni akawaambia: “Katika mwenye kula kukatoka chakula na katika mwenye nguvu kukatoka utamu.” Nyuma ya siku tatu hao vijana walikuwa bado hawajaweza kutegua hicho kitendawili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ