Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 15:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi, Yawe alimupatia Abiyamu mwana atakayetawala nyuma yake, kuwa taa ya kuangaza Yerusalema na kuuweka imara Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 15:4
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Mungu alipoangamiza miji katika bonde ambamo Loti alikuwa anakaa, alimukumbuka Abrahamu kwa kumutosha Loti katika miji hiyo, kusudi Loti asiangamizwe pamoja nayo.


kwa sababu Abrahamu alinitii mimi, akashika maagizo yangu, amri zangu, masharti yangu na sheria zangu.”


Lakini Abisayi mwana wa Zeruya alikwenda kumusaidia Daudi. Abisayi alimushambulia yule Mufilistini na kumwua. Kwa hiyo, watu wakamwapia Daudi wakisema: “Hautakwenda tena nasi katika vita, kusudi usiizime taa ya ufalme katika Israeli.”


Hata hivyo, kwa ajili ya baba yako Daudi, sitafanya hivyo wakati ungali unaishi, lakini nitauondoa utawala huo katika mikono ya mwana wako.


Lakini yeye, nitamwachia kabila moja kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi, na kwa ajili ya Yerusalema ambao nimeuchagua kuwa wangu katika makabila yote ya Israeli.


Huyo mwana wa Solomono nitamwachia kabila moja, kusudi wakati wote mutu mumoja wa uzao wa mutumishi wangu Daudi akuwe anatawala Yerusalema, akuwe taa inayoangaza siku zote mbele yangu katika muji ambao nimeuchagua ukuwe pahali pa kuniabudia.


lakini Yawe hakutaka kuangamiza ukoo wa Daudi kwa ajili ya agano alilokuwa amefanya na Daudi vilevile kwa sababu alikuwa ameahidi kwamba wazao wake wataendelea kutawala milele.


Humo nitamuchipukiza mufalme shujaa wa ukoo wa Daudi. Kama vile taa inayowaka, nitamwimarisha mufalme niliyemuchagua.


Wewe unawaokoa wanyenyekevu, lakini unawashusha wenye macho ya kujivuna.


Lakini juu ya Sayuni itasemwa: “Sayuni ni mama yao wote; Mungu Mukubwa atauimarisha.”


Basi watapewa jibu gani wajumbe wa taifa hilo? Wataambiwa: Yawe ameijenga imara Sayuni, na wamasikini kati ya watu wake watakimbilia kule.


musimupe hata nafasi ya kupumzika, mpaka atakapousimika Yerusalema, na kuufanya kuwa wenye sifa katika ulimwengu wote.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Yawe aliyeiumba dunia, Yawe aliyeifanya na kuiimarisha dunia, yule ambaye jina lake ni Yawe, anasema hivi:


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Ndio utakaowaangazia mataifa, na kuleta utukufu kwa watu wako Waisraeli.”


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Wayuda wamegeuka waadui za Mungu kwa sababu ya kukataa Habari Njema, na jambo hilo limekuwa faida kwenu ninyi watu wa mataifa mengine. Lakini wao ni wapendwa wake kufuatana na vile wamechaguliwa naye, kwa njia ya babu zao.


Kwa kuwa aliwapenda wazee wenu, yeye amewachagua ninyi wazao wao, akawatoa yeye mwenyewe katika inchi ya Misri kwa nguvu yake kubwa.


“Mimi Yesu, nimemutuma malaika wangu kwa kuwashuhudia maneno haya yote katika kanisa. Mimi ni wa shina na wa uzao wa mufalme Daudi. Mimi ni nyota ya asubui.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ