1 Wafalme 15:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200218 Halafu mufalme Asa akatwaa feza na zahabu yote iliyobaki katika hazina ya nyumba ya Yawe na katika hazina ya nyumba ya kifalme, akawapa watumishi wake, akawatuma Damasiki kwa Beni-Hadadi mwana wa Taburimoni, mujukuu wa Hesioni, mufalme wa Aramu, akasema: အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Yoasi mufalme wa Yuda alitwaa sadaka zote zilizotakaswa na babu zake wafalme wa Yuda: Yosafati, Yehoramu na Ahazia, na kuongeza zile zake, pamoja na zahabu yote iliyokuwa katika hazina ya nyumba ya Yawe na katika nyumba ya kifalme, akazituma kwa Hazaeli mufalme wa Aramu. Naye Hazaeli akatoka Yerusalema.