1 Abiyamu alianza kutawala kule Yuda katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa mufalme Yeroboamu mwana wa Nebati.
Nyuma, Rehoboamu alikufa na kuzikwa kwenye makaburi ya wazee wake, katika muji wa Daudi. Mama yake aliitwa Nama kutoka katika kabila la Waamoni, na mwana wake Abiyamu akatawala kwa pahali pake.
Kisha, akamwoa Maka binti ya Abusaloma, naye akamuzalia Abiya, Atai, Siza na Selomiti.