Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 13:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 maana Yawe aliniamuru nisikule chakula au kunywa maji, wala nisirudi kwa njia ileile niliyoifuata kwa kuja hapa.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 13:9
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku moja Yeroboamu alikuwa akisimama pembeni ya mazabahu kusudi afukize ubani. Basi, mutu wa Mungu kutoka Yuda akafika pale Beteli na ujumbe wa Yawe.


Basi, mutu yule akaenda zake, wala hakurudi kwa njia ile aliyoifuata kwa kuja Beteli.


Lakini yeye akamwambia: “Siwezi kurudi pamoja nawe, wala kuingia katika nyumba yako. Siwezi kula chakula au kunywa maji pahali hapa,


Basi, mutu wa Mungu akarudi pamoja naye, akakula chakula na kunywa maji kwa huyo muzee.


Lakini mutu wa Mungu akamwambia: “Hata kama ukinipa nusu ya urizi wako, sitakwenda pamoja nawe. Sitakula wala kunywa maji pahali hapa,


Sijaacha hata kidogo kushika amri yake; maneno yake nimeyatunza ndani ya moyo wangu.


Unikinge nisielekee kufanya mabaya, nisijishugulishe na matendo maovu, nisijiunge na watu wanaotenda mabaya, wala nisishiriki hata kidogo katika karamu zao.


Alipofika, akawaambia watu: Tafazali muondoke kwenye hema za watu hawa waovu na musiguse kitu chao chochote, musiangamizwe pamoja nao kwa sababu ya zambi zao zote.


Sasa kwa kuona munajua jambo hili, mutakuwa wenye heri kama mukilifanya.


Ninyi ni warafiki zangu, kama mukifanya sawa ninavyowaagiza.


Wandugu zangu, ninawasihi, mufanye angalisho na wale wanaoleta matengano na mambo ya kuwapotoa wengine wakipinga mafundisho muliyopokea. Mujitenge mbali nao.


Lakini niliwaandikia kwamba musishirikiane na mutu anayejiita ndugu mwamini, akiwa mwasherati, mwenye tamaa, mwenye kuabudu sanamu, mutukanaji, mulevi au munyanganyi. Na zaidi ya ile musichangie chakula na mutu wa namna hii.


Musishiriki katika matendo ya giza yasiyofaa, lakini muyafichue.


Kisha nikasikia sauti ingine kutoka mbinguni ikisema: “Mutoke katika muji ule ninyi watu wangu, kusudi musishiriki zambi zake na kupatwa vilevile na mapigo yatakayoupata.


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ