Unikinge nisielekee kufanya mabaya, nisijishugulishe na matendo maovu, nisijiunge na watu wanaotenda mabaya, wala nisishiriki hata kidogo katika karamu zao.
Musa na Haruni wakamwambia: “Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Tunakusihi utuache tujiendee katika jangwa mwendo wa siku tatu tutoe sadaka kwa Yawe, Mungu wetu. Kama sivyo, yeye atatuua kwa ugonjwa mukali au kwa upanga.”
Utamwambia ndugu yako Haruni mambo yote nitakayokujulisha. Naye Haruni ndugu yako, atamwambia mufalme wa Misri awaache Waisraeli watoke katika inchi yake.
Lakini Balamu akawajibu watumishi wa Balaki: Hata kama Balaki atanipa nyumba yake imejaa feza na zahabu, mimi sitaweza kuvunja amri ya Yawe, Mungu wangu, juu ya jambo lolote, dogo au kubwa.
Niliwaambia kwamba hata kama ungenipa nyumba yako imejaa feza na zahabu, mimi sitaweza kubadilisha agizo la Yawe, kwa kufanya jambo lolote, jema au baya kwa mapenzi yangu mwenyewe. Nilisema kwamba atakachosema Yawe ndicho nitakachosema.
Na nafasi yoyote watu watakapokataa kuwakaribisha na kuwasikiliza, mutoke kule na mukungute mavumbi toka juu ya miguu yenu. Jambo hili litakuwa ushuhuda juu yao.”