Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wafalme 13:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Basi, mufalme Yeroboamu akamwambia nabii: “Tafazali, umusihi Yawe, Mungu wako, uniombee mukono wangu upate kupona.” Naye nabii akamwomba Yawe, na mukono wa mufalme ukapona, ukarudia kwa hali yake ya zamani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wafalme 13:6
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mazabahu nayo ikabomoka, na majivu yake yakamwangika chini, kama kitambulisho kile yule mutu wa Mungu alichokitoa na ujumbe wa Yawe.


Ninataka kukupendeza kwa moyo wangu wote; unionee huruma kama ulivyoahidi!


Kwa hiyo sasa ninawasihi munisamehe zambi yangu mara hii, muniombee kwa Yawe, Mungu wenu, aniondolee kifo hiki.”


Mutwae makundi yenu ya kondoo na ngombe, muondoke. Muniombee na mimi baraka.”


Lakini hata mara hii mufalme wa Misri akafanya moyo wake kuwa magumu, wala hakuwaruhusu Waisraeli kuondoka.


Kisha mufalme wa Misri akamwita Musa na Haruni, akawaambia: “Musihi Yawe, kusudi aniondolee mimi na watu wangu vyura hawa, nami nitawaacha Waisraeli wajiendee na kutoa sadaka kwa Yawe.”


Basi, Musa na Haruni wakaondoka kwa nyumba ya mufalme wa Misri na Musa akamulilia Yawe amwondolee mufalme vyura wale aliomuletea.


Mumwombe Yawe maana ngurumo hii na mvua ya mawe vimezidi. Mimi nitawaacha muondoke na wala hamutabakia tena.”


Mufalme Zedekia aliwatuma Yehukali mwana wa Selemia, pamoja na kuhani Zefania mwana wa Maseya, kwa nabii Yeremia kusema awaombee kwa Yawe, Mungu wao.


Watu wa muji wa Beteli walikuwa wamewatuma Sareseri na Regemu-Meleki pamoja na watu wao kumwomba Yawe rehema zake,


Musa akamulilia Yawe akisema: Ninakusihi, ee Mungu, umuponye.


Basi, watu wakamwendea Musa, wakamwambia: Tumetenda zambi kwa kumunungunikia Yawe na wewe vilevile. Umwombe Yawe atuondolee nyoka hawa. Kwa hiyo, Musa akawaombea watu.


Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.


Halafu Yesu akasema: “Baba uwasamehe, kwa maana hawajui jambo wanalofanya.” Waaskari wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.


Kisha akapiga magoti, akalalamika, akisema: “Bwana, usiwahesabie zambi hii.” Na nyuma ya kusema maneno haya, akakufa.


Halafu Simoni akawaambia Petro na Yoane: “Muniombee ninyi wenyewe kwa Bwana, kusudi lisinipate hata neno moja kati ya maneno haya muliyosema.”


Mumwombe Mungu awabariki wale wanaowatesa; muwaombee baraka wala musiwalaani.


Usijiachilie kushindwa na ubaya, lakini ushinde ubaya kwa kutenda mema.


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


Hivyo wakamwambia Samweli: “Tafazali, utuombee sisi watumishi wako kwa Yawe, Mungu wako, kusudi tusikufe; kwa sababu tumezidisha zambi zetu kwa uovu huo wa kujitakia mufalme.”


Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ