Mutu huyo akaonyesha kitambulisho siku ileile, akasema: “Hiki ndicho kitambulisho Yawe alichosema: ‘Mazabahu hii itabomoka, na majivu yanayokuwa juu yake yatamwangika.’ ”
Mufalme Yeroboamu aliposikia maneno hayo ya mutu wa Mungu juu ya mazabahu kule Beteli, alinyoosha mukono akasema: “Mumukamate mutu yule!” Na mara moja ule mukono wake aliounyoosha, ukakauka, hakuweza tena kuukunja.
Basi, mufalme Yeroboamu akamwambia nabii: “Tafazali, umusihi Yawe, Mungu wako, uniombee mukono wangu upate kupona.” Naye nabii akamwomba Yawe, na mukono wa mufalme ukapona, ukarudia kwa hali yake ya zamani.
Na mapigano siku hiyo yakazidi kuwa makali, naye mufalme akiegemeshwa ndani ya gari, akiwaelekea Waaramu. Ilipofika magaribi, akakufa. Damu ikakuwa inamutoka kwenye kidonda chake na kutiririka mpaka chini ya gari.
Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.
Kama nabii akisema kitu aseme ni kwa jina la Yawe, na kitu hicho hakifanyiki au hakiko kweli, jambo hilo Yawe hakulisema; nabii amelisema kwa kiburi, nanyi musitishwe na jambo hilo.