12 Baba yao akawauliza: “Amefuata njia gani?” Nao wakamwonyesha njia yule mutu wa Mungu aliyoifuata kutoka Yuda.
Wakati ule, kulikuwa nabii mumoja muzee kule Beteli. Wana wake wakamwendea, wakamwelezea mambo yote yule mutu wa Mungu aliyotenda siku hiyo, kule Beteli. Wakamwambia vilevile yale maneno yule mutu aliyomwambia mufalme Yeroboamu.
Naye akawaambia watoto wake: “Munitayarishie yule punda.” Nao wakamutayarishia punda, na muzee akapanda juu yake.